Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Tuesday, May 27, 2014

Aacha Simanzi Na Majonzi Kwenye Familia Yake Baada Ya Kufariki Kwa Kunywa Sumu

 
Oscar enzi za uhai wake.

MOSHI kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Oscar John Njau mwenye umri wa miaka 24 ambaye alikuwa ni dereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda, mkazi wa rau madukani, mjini Moshi  amefariki dunia baada ya kunywa sumu. Tukio hilo la kustajabisha lilitokea jana tarehe 26 Mei 2014 majira ya saa saba mchana.

Maelezo kutoka kwa ndugu waliokuwa wanaishi nyumba moja na Oscar wanasema kuwa siku ya tukio Oscar aliamka asubui na kujiandaa na kuelekea kwenye shuhuli zake za kuendesha  bodaboda kama ilivyo kawaida yake. Lakini ilipofika majira ya saa nne abuhi, Osca alirejea nyumbani na kuiegesha pikipiki yake kisha akawa anazunguka zunguka eneo la nyumbani.

Baada ya muda kidogo alielekea nyuma ya choo ambapo inadaiwa kuwa ndipo ilipokuwa imehifadhiwa sumu hiyo na kuichukua na kuamua kunywa na baada ya hapo alielekea kwenye duka lililopo karibu na nyumbani kwao na kununua pombe inayohifadhiwa kwenye mfuko mdogo maarufu kama kiroba na kuanza kunywa.

Baada ya kunywa kiroba alianza kutapika na kwa watu waliokuwa hapo dukani wanasema alikuwa akitapika matapishi yaliyokuwa na harufu kali sana ya aina ya sumu aliyokuwa amekunywa, ndipo watu wale wakashtuka na kuamua kuwaita ndugu zake na Oscar. Ndugu zake walipofika walimuangalia Oscar na kutokana na hali aliyokuwa nayo wakawa na wasiwasi kuwa alikunywa sumu na walipo muuliza Oscar alikiri kuwa kweli amekunywa sumu. 
Ndugu zake wakafanya juhudi za kumtapisha na baadae kuamua kumpeleka hospitali ya rufaa ya Mawenzi, baada ya kufika hospitalini wauguzi walifanya jitihada za kuokoa maisha ya Oscar kwa kumpa dawa na kumtapisha sumu lakini juhudi za wauguzi hazikufanikiwa kwakuwa sumu ilisha sambaa mwilini kwa kiasi kikubwa sana. Na ilipofika majira ya saa saba mchana Oscar alifariki.

Sababu zilizompelekea Oscar kuamua kunywa sumu mpaka sasa hazijafahamika vizuri, japo kuna tetesi zisizo rasmi kuwa ni maneno yaliyokuwa yakiongelewa na mama yake wa kambo, na ni maneno ambayo hayakumfurahisha Oscar. Mtandao huu wa king Jofa bado unafuatilia ili kuweza kufahamu ukweli zaidi.

Na taarifa kutoka kwa ndugu wa Oscar ni kwamba atazikwa siku ya ijumaa ya tarehe 30 Mei 2014.
Timu nzima ya King Jofa inawapa pole ndugu, jamaa na marafiki wa Oscar John Njau.

No comments:

Post a Comment