Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, June 14, 2014

HAYA NDIO MAMBO MUHIMU YALIYOZUNGUMZWA KATIKA SIKU YA UCHANGIAJI DAMU NCHINI

MOSHI meneja wa kituo cha damu salama kanda ya kaskazini  Dr. Wilhelmuss Mauka,  amesema kutokuwa na damu katika hospitali ni urasimu wa wauguzi   pamoja na njaa za manesi  kuwataka wagonjwa kulipia damu hiyo huku damu hiyo ikitolewa  bure.

Dr. Mauka alisema hayo jana katika siku ya uchangiaji damu nchini, iliyofanyika katika  viwanja vya ofisi vya  benki ya damu KCMC manispaa ya moshi mkoani Kilimanjaro.

Alisema wagonjwa wanapotozwa fedha ili wawekewe  damu  ni kosa na kwamba damu iko nyingi na hutolewa bure kama wananchi wanavyochangia.

“kulipia damu kwenye mahospitali ni kosa damu inatolewa bure katika hospitali zote bila kubagua ya serikali na binafsi wanachokifanya wauguzi kutoza wagonjwa damu hiyo ni kosa na ni urasimu tu unakuwapo katika hospitali husika." alisema Mauka.

Dr. Mauka alisema damu katika kituo hicho ipo yakutosha na kwamba kituo hicho hakijawahi kupungukiwa na damu, na kwamba kila mwaka huwa wanavuka malengo ya ukusanyaji wa damu kwa asilimia  mia moja.

Kwa upande wake mgeni rasmi ambaye ni Daktari wa chuo cha polisi moshi Francis Ngozi, alisema wamekuwa wakihamasisha polisi kuchangia damu  ili kuokoa maisha ya watu haswa wale wanapoata ajali za barabarani.

 Dr. Ngozi alisema  kutokana na kuwapo na ajali nyingi za barabarani haswa zaitokanazo na bodaboda  ni vyema jamii ikajitokeza kuchangia damu ili kuweza kuokoa maisha ya wananchi.

No comments:

Post a Comment