MOSHI shirika
la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoani Kilimanjaro
limetoa sare za shule kwa wanafunzi 25
yatima na wanaoishi katika mazingira mgumu, wanafunzi hao wanaosoma katika shule ya msingi Mwenge
iliyopo manispaa ya moshi.
Akikabidhi sare hizo kaimu meneja wa NSSF mkoani Kilimanjaro Albert
Kibonde, alisema >> "Shirika hilo limekuwa likitoa msaada kwa watu wenye
uhitaji hasa wale wanaoishi katika mazinga magumu na hatarishi."
Kibonde alisema mchango wa huo umetoka kwa wafanyakazi wa NSSF na kwamba
kila mwaka wanatoa mchango kwa jamii yenye mahitaji na wasiojiweza, pamoja na
wale wenye mahitaji muhimu.
“Sisi kama wafanyakazi wa NSSF huwa tunachanga fedha kwa ajili ya kusaidia watu ambao hawana uwezo na tumeona kwa awamu hii tuwapatie sare
watoto ambao wanaishi katika mazingira magumu” alisema Kibonde
Kwa upande wake mkuu wa shule ya
msingi mwenge Pasfia Ernest, alishukuru shirika NSSF kwa kusaidia watoto hao
sare za shule na kwamba wanafunzi hao
wametoka katika familia duni ambazo zinashindwa kuchangia chochote.
Ernest alisema shule hiyo ina
jumla ya watoto 25 ambao hawana uwezo na kwamba hata madaftari huwa wananunuliwa na shule hiyo.
“Watoto hawa huwa wanalele na bibi
na wengine na majirani na watu ambao
wanaishi na watoto hawa nao hawana uwezo mara nyingi shule ndio inayowatimizia
mahitaji yao ya shule kwa kutumia faida inayopatikana katika duka la shule”
alisema mkuu huyo.
No comments:
Post a Comment