Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, June 14, 2014

JESHI LA POLISI LATOA TAHADHARI KWA MASHABIKI WA SOKA KIPINDI CHA KOMBE LA DUNIA

SIHA jeshi la Polisi wilayani Siha mkoani Kilimanjaro limewatahadharisha wananchi wote hasa mashabiki wa mpira wa miguu maarufu kama soka kuwa makini na vitendo vya uhalifu vinavyaweza kujitokeza katika wakati huu wa fainali za michezo ya kombe la Dunia lililoanza tarehe 12 Juni 2014 huko nchini Brazili.

Tahadhari hiyo imetolewa leo na mkuu wa Polisi Wilaya ya Siha [OCD] Lutusyo Mwakyusa wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu usalama wa raia na mali zao kutokana na kuanza kwa michuanao ya kombe la Dunia ambapo kwa kiasi kikumbwa michezo hiyo hufanyika nyakati za usiku

Mwakyusa alisema kufuatia kuanza kwa kombe la dunia na kutambua kwamba michuano hiyo inatazamwa na watu wengi katika maeneo mbali mbali kupitia Luninga Jeshi hilo linatoa tahadhari kwa wananchi wote hasa mashabiki wa michezo hiyo kuwa makini na vitendo vya kihalifu vinavyoweza kujitokeza katika kipindi hicho

Aidha aliwataka wamiliki wa Kumbi mbalimbali, Bar na sehemu mbali mbali zinazotumika kuonesha michuano hiyo wametakiwa kuzingatia uhalali wa vibali vyao ikiwamo kuwa makini na vitendo vyovyote vitakavyo ashiria uhalifu na kutoa taarifa kwa vyombo usika

Mbali na kutoa taarifa za uhalifu pia wametakiwa kuzingatia hali ya usalama ndani ya ukumbi kwa kuweka madirisha makumbwa ili watazamaji waweze kupata hewa safi ili isije tokea kama ilivyotokea huko Tabora miaka ya hivi karibu ambapo watu kadhaa waliumia kutokana na msongamano mkubwa wa watu.

Pia Wananchi wote wanapaswa kuwa makini na mali zao wakati wote wa michuano hiyo kwa kuweka ulinzi katika makazi yao kuimarisha falsafa ya ulinzi shirikishi inayoimiza kutoa taarifa pindi unapoona kiashiria chochote cha uhalifu iwe nyumbani kwako au kwa jirani yako.

No comments:

Post a Comment