Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Tuesday, June 17, 2014

MLIMA KILIMANJARO UMEPOTEZA TAKRIBANI ASILIMIA 80 YA THERUJI

MLIMA mrefu kuliko yote na wenye heshima kubwa dunia nzima na mlima unaoipatia serikali ya Tanzania mapato makubwa sana    kutokana na watu wa ndani na nje ya Tanzania kupanda mlima huo mrefu kuliko yote Afrika, mlima Kilimanjaro una urefu wa mita 5,895 (futi 19,340). Mlima Kilimanjaro wenye vilele vitatu Kibo, Mawenzi na Shira. Mlima Kilimanjaro umepoteza takribani asilimia 80 ya theruji yake kuanzia mwaka 1912 kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.

Kauli hiyo ilitolewa bungeni Dodoma, na Naibu Waziri nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Ummy Mwalimu alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Ole, Rajabu Mbarouk Mohamed (CUF).

Mbunge huyo alitaka kujua kuwa tathmini inaonyesha ni kiasi gani cha theruji kilichopungua kutokana na athari ya mabadiliko ya tabia nchi.  Aidha katika swali la nyongeza Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini, (CHADEMA), amesema wazee ambao wamepanda miti miaka 20 iliyopita wanakatazwa kukata miti yao kwa ajili ya shughuli mbalimbali.

Mbunge huyo amehoji Serikali inasemaje kuhusiana na jambo hilo.

Akijibu maswali hayo kwa pamoja, Mwalimu amesema kulingana na jopo la wanasayansi wa mabadiliko ya tabia nchi, Mlima wa Kilimanjaro umepoteza takribani asilimia 80 ya theruji yake kuanzia mwaka 1912 kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.

Amesema Serikali na Jumuiya za kimataifa zimekuwa zikichukua hatua mbalimbali katika kukabiliana na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabia nchi ikiwa ni pamoja na kusaini/kuridhia mkataba wa mabadiliko ya tabia nchi wa mwaka 1992.

Ameongeza kuwa Serikali ilisaini na kuridhia Itifaki ya Kyoto chini ya mkataba huo, kuandaa sera, sheria na mikakati mbalimbali. Kwa upande wa wazee kunyimwa kukata miti yao, amesema ni kweli kuna changamoto hiyo katika maeneo mbalimbali na kuwataka kufuata utaratibu ili kupata kibali cha kukata miti.

No comments:

Post a Comment