Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Tuesday, June 17, 2014

ASKOFU AWATAKA WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA KUJADILI MASWALA YENYE TIJA

WAJUMBE wa bunge la katiba, wametakiwa kuacha kutumia muda mrefu kujadili masuala ambayo hayana tija kwa jamii,  badala yake kujikita zaidi katika  masuala ambayo yatalisaidia taifa na jamii kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa na Askofu mkuu wa dayosisi ya Mashariki na Pwani, Stanley Hotay, katika jubilee ya kuadhimisha  miaka 75, tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo na sherehe ambazo ziliendana  sambamba na harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa kanisa hilo.

Askofu Hotay amesema kanisa haliko tayari kuona  kuna kuwepo na makundi  ya wawakilishi walioko ndani ya bunge la katiba wanakuwa wapiganaji ambao wanahamamisha ubaguzi ndani ya Tanzania.

Askofu huyo amewataka wajumbe wa bunge la katiba kuzingatia maadili na maamuzi yao yawe yenye tija kwa wananchi ili kuweza kupatikana katiba iliyo na manufaa bora.

Hata Askofu Hotay,  ameongeza kuwa,  wajumbe hao wanatakiwa kutambua kuwa wanatumia fedha za wananchi ambao ni wa hali ya chini  kulipwa posho zao huku wakiendelea kususia na kutoka ndani ya bunge hilo.


Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Shinyanga Anna Rose Nyamubi ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo, amewataka wananchi  pamoja na viongozi wa dini kucha kushabikia wanasiasa wenye lengo la kutumia mchakato wa upatianaji wakatiba mpya kuvuruga amani.

Akisoma risala kwa mgeni rasmi mchungaji kiongozi wa kanisa la Angalika Majengo Alfredy Kanyarukiga, amesema zaidi ya shilingi bilioni moja zinahitajika katika ujenzi wa kanisa hilo na kwamba, hadi kukamili kwa kanisa hilo litaweza kuchukua waumini zaidi ya elfu moja.

No comments:

Post a Comment