Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, June 26, 2014

POLISI MKOANI KILIMANJARO INAWASHIKILIA WATU WAWILI WANAOSHUKIWA KUWA NI MAJAMBAZI

Kamanda Boaz akiwa ameshikilia silaha ambazo zinaaminika zilikuwa zikitumika kwenye matukio ya ujambazi.

Watu wawili waaoshukiwa kuwa ni majambazi wamekatwa na jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro wakiwa na bunduki mbili aina ya short gun zikiwa zimekatwa mtutu ambazo zinakisiwa kuwa ndizozilizokuwa zikitumika katika matuio mbalimbal ya kiuhalifu katika mkoa wa Kilimanjaro.

Akidhibitisha kukamatwa kwa majambazi hao kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Robert Boaz amesema kukamatwa kwao kunatokana na jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro kuanza msako mkali, baada ya kuongezeka kwa matukio ya uhalifu ukiwemo wa kutumia ya silaha.

Kamanda Boazi amewataja watuhumiwa hao ni Ibrahimu Machaku mkazi wa kijiji cha kahe wilayani Moshi aliye kamatwa na silaha ambayo inasadikiwa kuibwa katika chama cha ushirika cha legomulo wilayani Moshi, pia wamemkamata Laurenti Massawe mkazi wa jiji la Arusha alipovamia na kuiba nyumbani kwa mfanyabiasha mmoja Bw Mehboo Sadik eneo la shant town mjini moshi akiwa na bunduki aina ya short gun iliyokatwa mtutu.

Aidha kamanda Boaz ameseama jeshi hilo pia limefanikiwa kukamata madawa yanayosadikiwa kuwa ni ya kulevya aina ya cocan ambayo yalikuwa yametelekezwa ndani ya ndege ya Ethiopia air line katika kiwanja cha KIA kilichopo mkoani Kilimanjaro na kwamba jeshi hilo linaendelea na uchunguzi wakumpata muhusika wa madawa hayo.

No comments:

Post a Comment