HAI zaidi ya vijiji 11 wilayani Hai
mkoani Kilimanjaro vikiwemo vijiji vya Mungushi, Mtakuja, Tindigani na Mlima
shabaha vinatarajia kunufaika na huduma ya umeme kupitia wakala wa umeme
vijijini REA huku vijiji vitakavyofuatia mara baada ya kukamilika kwa awamu
hiyo ni vijiji vya chemka, kambi ya nyuki, kilimambogo, mbatakero pamoja na
mudio.
Hayo yamebainishwa hii leo na meneja
wa Tanesco wilaya ya Hai Bw. James Chinula wakati wa uwasilishaji wa mada
katika kikao cha baraza la wafanyabiashara wilaya ya Hai kilichofanyika katika ukumbi wa
idara ya maji Wilayani Hai.
Bw. Chinula alisema kuwa baada ya kupatikana kwa substation mpya ya Kia na kukidhi mahitaji ya wilaya ya Hai zaidi ya vijiji 11 vitapatiwa huduma hiyo kwa awamu ya kwanza huku akibainisha kuwa moja ya changamoto za shirika la umeme Tanesco-Hai ni zaidi ya 50% ya nguzo za umeme ni chakavu na hivyo kuwa changamoto katika utoaji wa huduma.
Bw. Chinula alisema kuwa baada ya kupatikana kwa substation mpya ya Kia na kukidhi mahitaji ya wilaya ya Hai zaidi ya vijiji 11 vitapatiwa huduma hiyo kwa awamu ya kwanza huku akibainisha kuwa moja ya changamoto za shirika la umeme Tanesco-Hai ni zaidi ya 50% ya nguzo za umeme ni chakavu na hivyo kuwa changamoto katika utoaji wa huduma.
Kwa upande wa wafanyabiasha bw. Johnson Mtey amesema kuwa elimu ya matumizi sahihi ya mashine za EFD itolewe ili kuondoa dhana iliyopo miongoni mwa wafanyabiashara juu ya matumizi ya mashine hizo jambo ambalo bw. Rutagwelera amesema kuwa mbali na semina zilizotolewa bado elimu zaidi inaendelea kutolewa.
Awali akifungua kikao hicho Mkuu wa
Wilaya ya Hai ndugu Novatus Makunga ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa baraza
hilo amesema kikao hicho ambacho sasa kitakuwa kinafanyika mara kwa mara
kimelenga kujadili fursa na changamoto za biashara zilizopo kwa lengo la
kuimarisha na kukuza biashara na kuongeza ushirikiano baina ya sekta binafsi na
sekta za Umma ili kuongeza ufanisi katika kazi.
No comments:
Post a Comment