Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, June 21, 2014

WATANO WAFIKISHWA KIZIMBANI KWA KOSA LA KUMLAWITI MTOTO WA MIAKA 16

WATU watano wakiwemo wanawake wawili wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 16.
 Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka katika kesi hiyo Beatus John, washtakiwa hao, Charles Atanadi Kiule, January Alaji, Patrick Sapisi, Khadija Salum na Namwaka Mbwana, wanadaiwa kutenda kosa hilo mwezi Novemba, mwaka jana (2013), eneo la Lembeni, wilaya ya Mwanga, ambapo walimlawiti kijana huyo ambae jina lake linahifadhiwa.
Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka huyo, katika shtaka la kwanza, washtakiwa Charles Atanadi Kiule, January Alaji na Patrick Sapisi, kwa pamoja walimlawiti kijana huyo kwa zamu.
Aidha alisema katika shtaka la pili, watuhumiwa hao wawili wanashtakiwa kwa kumjeruhi kijana huyo kwa kumchapa kwa fimbo na nyaya na kusababishia maumivu makali na majeraha sehemu mbalimbali za mwili wake.
Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka huyo watuhumiwa Khadija Salum na Namwaka Mbwana, wanakabiliwa na shtaka moja tu la kushawishi washtakiwa wa kwanza hadi wa watatu kumbaka kijana huyo kwa madai kuwa alitaka kumbaka mtoto wa mshtakiwa wa nne, Khadija Salum.

Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo Emmanuel Gasper, aliiambia mahakama hiyo kuwa watuhumiwa hao wana kesi ya kujibu ambapo aliihairisha  kesi hiyo hadi Julai 2, mwaka huu.
Aidha wastakiwa namba nne na namba tano wanatarajiwa kutetewa Rehema Mtuli kutoka  jijini Dar es salam huku wastakiwa namba moja hadi tatu hawana wakili wa kuwatetea.
upande wa mashtaka unatarijiwa  kuleta mashahidi nane. Washtakiwa wote wako nje kwa dhamana.

No comments:

Post a Comment