Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, June 2, 2014

WATU WATATU WAFARIKI DUNIA KATIKA MATUKIO TOFAUTI MKOANI KILIMANJARO

WATU watatu wamefariki dunia mkoani Kilimanjaro katika matukio matatu tofauti, likiwemo tukio la mtu mmoja kujiua kwa kujinyonga na chandarua cha kuzuia mbu akiwa chumbani kwake.
Akithibitisha kutokea kwa matukio hayo Kaimu Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Koka Moita alisema tukio la kwanza lilitokea Juni 1, mwaka kuu, majira ya saa  8:00 mchana katika kijiji cha  Kilema, Moshi Vjijini, mkoani Kilimanjaro.
Akielezea mazingira ya tukio hilo kamanda Moita alisema Martin Michael, (45) alikutwa akiwa amening’inia kwenye paa la chumbani kwake akiwa amejinyonga kwa kutumia chandarua cha kuzuia mbu kilichokuwa kimetundikwa kwenye kitanda alichokuwa akikitumia kulala.
Aidha kamanda huyo alisema chanzo cha kifo hicho hakijajulikana na kwamba jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro linaendelea na uchunguzi ili kubaini ukweli kuhusu chanzo cha tukio hilo na kwamba mwili wa marehemu huyo umehifadhiwa katika chumba cha maiti kilichopo katika hosptali ya Kilema.
Kamanda Moita alisema katika tukio la pili mwanamke mmoja aliemtaja kama Namkondo Hassani, (35) mkazi wa kijiji cha Msufini Kata ya Ndungu, wilayani Same, alikutwa amekufa katika mfereji wa unaotumika kwa umwagiliaji katika kilimo.
 
Aidha kamanda huyo alisema katika tukio la tatu Juni 1, mwaka huu, mtu mmoja aliemtaja kama Devotha Deusi, (24), alikutwa amekutwa amefariki dunia nyumbani kwake eneo la Mdawi, Old Moshi.
Kamanda Moita alisema kuwa maiti ya mwanamke huyo ilikutwa majira ya saa saba za mchana wa siku hiyo na kwamba uchunguzi wa awali unaonyesha ya kuwa alifariki kutokana na ugonjwa uliokuwa ukimsumbua kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment