Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, June 2, 2014

IDADI YA WAGONJWA WA DENGUE YAFIKIA 5 NA WENGINE 11 HATARINI MKOANI KILIMANJARO

MOSHI idadi ya wagonjwa wenye homa ya dengue, katika Manispaa ya Moshi imeongezeka na kufikia wagonjwa watano, huku wengine 11 wamegundulika kuwa na ugonjwa huo.

Hayo yamesemwa na Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Dkt Christopha Mtamakaya wakati  akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake .

Dkt. Mtamakaya amesema wagonjwa watatu wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mawenzi,  huku wengine wawili wakiwa katika hospitali ya Jaffari,  na wagonjwa 11 waliogundulika kuwa na dalili hizo uchukuaji wa sampuli za damu unaendelea kufanyika katika hospitali hiyo.


Hata hivyo Dkt mtamakaya ametoa  rai kwa wananchi kuacha kutumia dawa bila kupima, pindi wanapojihisi kuumwa, na kwamba juhudi zinaendelea kuchukuliwa na wataalamu wa afya ili kudhibiti ugonjwa huo kwa kuua mazalia ya mbu.

Aidha Dkt Mtamakaya amewaomba wananchi waendelee kufanya usafi wa mazingira, kufukia madimbwi na maji machafu pia kutumia chandarua na kufika hospitalini pindi wanapoona dalili za kuumwa.

No comments:

Post a Comment