Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, August 22, 2014

DIWANI WA KATA YA MASAMA ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA HAI.

HAI baraza la Madiwani la halmashauri ya Wilaya ya Hai, Mkoani Kilimanjaro limemchagua Ally Mwanga ambae ni Diwani wa kata ya Masama Mashariki (CCM) kuwa makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kwa kipindi cha kuanzia Julai 2014 hadi June 2015. 
Mwanga alichaguliwa kwa kupigiwa kura za siri za ndio au hapana baada ya mgombea wa Chama cha Demokransia na Maendeleo (CHADEMA) kujitoa kutokana na maridhiano walikubaliana wajumbe wa baraza hilo linaloundwa na vyama viwili vya Siasa vya CCM na CHADEMA. Uchaguzi huo wa kumchagua makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo ulifanyika katika ukumbi wa Halamashauri ambapo vyama hivyo viwili vilikubaliana nafasi ya makamu mwenyekiti iendelee kushikiliwa na diwani wa CCM kutokana na kuongozwa na Mwenyekiti anayetoka CHADEMA. Awali akitangaza matokeo hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Melekzedeck Humbe alisema Mwanga alipata kura 18 kati ya 19 zilizopigwa huku moja ikiharibika. Baraza hilo la madiwani pia liliwachagua wajumbe na wenyeviti mbalimbali wa kamati watakao ongoza kwa pindi cha mwaka mmoja cha kuanzia Agosti 2014 hadi June 2015.

No comments:

Post a Comment