Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, August 22, 2014

ZIARA YA MAGWIJI WA MPIRA ULIMWENGUNI REAL MADRID MKOANI KILIMANJARO

d8f4b35c644f0423a21a23076ac82592
Kuanzia kushoto, Luis Figo, Zinedine Zidane na Ronaldo de Lima enzi hizo wakicheza Real Madrid - See more at: http://shaffihdauda.com/?p=3927#sthash.mdYMdq4X.dpuf
Kuanzia kushoto, Luis Figo, Zinedine Zidane na Ronaldo de Lima enzi hizo wakicheza Real Madrid - See more at: http://shaffihdauda.com/?p=3927#sthash.mdYMdq4X.dpuf
Kutoka kulia ni Ronaldo De Lima, Zinedine Zidane na Luis Figo, enzi wakichezea Real MAdrid
Kuanzia kushoto, Luis Figo, Zinedine Zidane na Ronaldo de Lima enzi hizo wakicheza Real Madrid - See more at: http://shaffihdauda.com/?p=3927#sthash.mdYMdq4X.dpuf

Kuanzia kushoto, Luis Figo, Zinedine Zidane na Ronaldo de Lima enzi hizo wakicheza Real Madrid - See more at: http://shaffihdauda.com/?p=3927#sthash.mdYMdq4X.dpuf
MOSHI timu ya Real Madrid ya nchini Hispania, inatarajia kuwasili mkoani Kilimanjaro, Agosti 24, mwaka 2014 lengo likiwa ni kutangaza fursa za utalii zilizopo mkoani Kilimanjaro hususani katika mlima Kilimanjaro. 

Akitoa taarifa kwa wanahabari mkoani Kilimanjaro, mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama, alisema ziara ya wachezaji hao itatoa mwanya kwa wachezaji wengine kuja hapa nchini Tanzania na kuweza kuzitembelea hifadhi zilizopo hapa nchini.

Alisema uongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kwa kushirikiana na wadau wa michezo wamejiandaa vyema katika kuwapokea wachezaji hao, na kuongeza kuwa mkoa umejiandaa vyema katika kuwakarimu wachezaji hao wa Real Madrid.

Gama alisema kuwa licha ya wachezaji hao kuja na kutembelea hifadhi ya mlima Kilimanjaro pia itatoa fursa ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo mkoani Kilimanjaro, na kwamba mkoa umeandaa ratiba ambayo itawafikisha hadi kwenye mlima Kilimanjaro na kupata maelezo kuhusu mlima mrefu kuliko yote barani Afrika.

Pia mkuu wa mkoa alisema baada ya kufika eneo la mlima Kilimanjaro, watapata fursa ya kupanda kwa umbali kidogo ili kujionea mandhari ya mlima huo jinsi ulivyo kisha kupata maelezo ya jinsi safari ya kuanza kuupanda mlima huo inavyofanyika.

Aidha alifafanua kuwa uongozi wa mkoa umeuagiza uongozi wa hifadhi ya mlima Kilimanjaro (KINAPA), kuandaa maelezo yatakayowawezesha wachezaji hao kushawishika kurudi tena kama watalii. Kwa mujibu wa ratiba ya ziara ya wachezaji hao baada ya kupanda mlima Kilimanjaro, watapata chakula cha mchana kabla ya kurudi mjini Moshi ambapo wanatarajia kuwa wageni rasmi katika mechi ya kirafiki kati ya mabingwa wa mkoa wa Kilimanjaro Panone FC na timu ya soka ya Machava ya mjini Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment