Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, August 8, 2014

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AWASHAURI WANANCHI KUJIWEKEA AKIBA YA CHAKULA

KILIMANJARO serikali mkoani Kilimanjaro imewataka wananchi kujiwekea akiba ya chakula katika kipindi hichi cha mavuno na kuacha kutumia nafaka kwa kutengenezea pombe za kienyeji, lengo likiwa ni kukabiliana na kipindi cha njaa.

Mkuu wa mkoa wa kilimnjaro Leonidas Gama, aliyasema hayo wakati akizungumza na mmoja muandishi wa mtandao huu jana Mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro ambapo alisema hali ya kilimo na upatikanaji wa chakula ni ya kuridhasha.

Alisema mkoa wa Kilimanjaro  baadhi ya wilaya zake zimekuwa zikikabiliwa na njaa kutokana  na wananchi kutokuwa na desturi ya kujiwekea akiba ya chakula katika kipindi cha mavuno na kutumia nafaka katika utengenzaji wa pombe za kienyeji.

Alisema  mkoa ulijiwekea malengo ya kuvuna na kukusanya zaidi ya tani Milioni 1.9 katika kipindi cha   mwaka 2013/2014 na kwamba hali ya upatikaji   wa chakula ni ya kuridhisha ambapo katika kipindi cha mwaka 2014 wanatarajia kuvuna kuvuka lengo hilo.
 
Aidha aliziagiza halmashauri za wilaya  kupitia wataalamu wa kilimo mkoani Kilimanjaro kuwaelimisha wananchi juu ya njia bora za kuhifadhi  mazao ili kusaidia vyakula hivyo kuto haribika kwa haraka.

No comments:

Post a Comment