Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, September 5, 2014

UKOSEFU WA HUDUMA ZA AFYA ZA KISASA NA UHAKIKA ZADAIWA KUWA SABABU KUBWA YA WATANZANIA KUFUATA HUDUMA HIYO NJE YA NCHI

Mkurugenzi mtendaji wa hospitali za Apollo Dr. Hariprasad akiwahutubia wadau wa afya hivi karibuni. Hospitali ya Apollo inaamini katika kutoa huduma bora kwa wateja wake.

Dar es Salaam, Septemba, 2014. Ukosefu wa huduma za afya za uhakika na za kisasa zinadaiwa  kuwa sababu kubwa ya watanzania  wengi kufuata huduma hizo nchi za nje.
Hospitali ya Apollo ilikuwa moja ya hospitali za mwanzo kabisa katika bara la Asia, na duniani kwa ujumla kuleta huduma zote za kiafya chini ya paa moja. Na kwa wakati huu, mpango huo kabambe umeifanya hospitali hiyo kufanikiwa katika Nyanja zote za matibabu.
Dr. Prathap C Reddy, muasisi wa huduma za kiafya za kisasa nchini india, alianzisha hospitali ya aina yake nchini humo mwaka 1983. Ikitoa huduma zote za kiafya, hospitali ya Apollo ina zaidi ya vitanda 8000 katika jumla ya hospitali zake zipatazo 50, na idadi ya maduka ya dawa baridi yapatayo 50, vituo vya afya vya uchunguzi wa kina, vituo vya bima za afya pamoja na uchunguzi wa kina wa seli mbalimbali kwa ajili ya utafiti. Hospitali ya Apollo ni hospitali bingwa duniani kwa upandikizi wa viungo mbalimbali vya binadamu duniani. 
Nchini Tanzania, magonjwa yasiyo ya kuambukiza, kama saratani,kisukari, na magonjwa yanahusiana na moyo yamekuwa yakiongezeka kwa kasi. Magonjwa haya yamesababisha kupotea kwa nguvu kazi ya taifa na pia yanagharimu fedha nyingi ambazo zingeweza kutumika kuboresha shughuli nyingine za kiuchumi.

Hivi sasa, uwezo wa Tanzania kutibu magonjwa ya moyo, upasuaji wa moyo, saratani, na matatizo ya figo ni mdogo, na maelfu ya watanzania hufuata huduma hizi nje ya nchi kwa bei nafuu, hususani nchini India.

Ugonjwa wa moyo ni wa pili kwa kusababisha vifo vingi nchini Tanzania baada ya malaria, ukichangia vifo 287 kwa siku, au 104,755 kwa mwaka, kwa takwimu za taasisi ya moyo Tanzania. ‘Tanzania kwa sasa haina kituo  maalum cha kutoa matibabu ya jumla ya moyo. Asilimia 20 ya vifo vyote hutokana na ukosefu wa utaalamu, vifaa na umaskini, na wale wenye uwezo inawabidi kusafiri nje ya nchi,’ 

Inaongeza taasisi hiyo katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, safari ya hospitali ya Apollo imetengeneza historia ya kupendeza katika hali nzima ya utoaji wa huduma za kisasa za afya nchini India. Taasisi hiyo imeendelea kung’ara kati ya watoa huduma binafsi. Hospitali hii ilikuwa moja ya waanzilishi wa tuzo za juu za utoaji wa huduma ya kisasa duniani.


Hospitali ya Apollo ni moja ya hospitali zinazojulikana vyema miongoni mwa wa-Tanzania, kwani viongozi wengi maarufu, wafanyabiashara na mamia ya wagonjwa wenye uhitaji wa upasuaji wamekuwa wakisafiri na kupata matibabu kutoka hospitali hizi maarufu.

Hivi karibuni hospitali ya Apollo ilifanya upasuaji wa kuwatenganisaha mapacha kutoka Tanzania kwa mafanikio makubwa.

Nchi za India na Tanzania zimekua na ushirikiano mkubwa kihistoria, kiutamaduni, kisiasa na kibiashara, na uwepo wa  hospitali hizo nchini Tanzania utaendelea kudumisha uhusiano mwema kati ya nchi hizi mbili.

Zaidi kuhusu hospitali za Apollo
Hospitali ya Apollo ilifunguliwa mnamo mwaka 1983, na kutoka kipindi hicho imekuwa ikiendeshwa kwa kauli mbiu isemayo "Dhamira yetu ni kuleta huduma ya kisasa karibu kabisa na walengwa. Tunajitolea kutoa huduma bora na mafanikio katika elimu na  utafiti kwa ajili ya jamii  ya kibinadamu".

Katika miaka 30  tokea kuanzishwa kwake, hospitali ya Apollo imeandika historia kubwa kupata kuonekana nchini India. Ni moja ya kampuni kubwa ya Afya katika bara la Asia, na pia imeleta mapinduzi makubwa katika sekta ya afya nchini india.

Katika safari yake, imeweza kuboresha maisha ya watu wapatao milioni 39 kutoka nchi 120.
Inatoa huduma maalum 52 na vitanda vya upasuaji 710
Imefanya upasuaji wa moyo wenye kufikia idadi ya watu 152,000 na panuzi 125, 000 za mishipa myembamba.
Imefanya upasuaji wa wa viungo unaopita kiasi cha idadi ya watu 10,000, upasuaji wa uvimbe wa ubongo, uti wa mgongo na zaidi.

Taasisi ya Apollo ni moja ya taasisi zinazoongoza nchini india, zikiwa na teknolojia za kisasa kama Novalis TX, PET MRI na Upasuaji unaotumia mashine za kiroboti.

No comments:

Post a Comment