Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, September 8, 2014

Shirika la UNDP latoa shilingi milioni 39 kusaidia shirika la TEACA kuendeleza mradi wa mazingira


Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, (UNDP), limetoa fedha kiasi cha shilingi milioni 39, kwa Shirika lisilo la kiserikali la TEACA, kwa lengo la kuendeleza mradi wa mazingira,  katika mtandao wa vijiji 37 ili kuweza kurejesha uoto wa asili ambao umeanza kupotea katika hifadhi ya Mlima Kilimanjaro.


Makamu Mwenyekiti wa shirika hilo, Adoncome Mcharo, ameyasema hayo wakati akitoa taarifa ya maendeleo ya shirika hilo, kwenye mkutano mkuu wa 18 wa shirika hilo.


Amesema taasisi hiyo imekuwa ikiendelea na shughuli zake za kupambana na kuhifadhi wa mazingira na kuyaendeleza  ikiwa ni pamoja na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa mazingira bora kwa viumbe hai.

Mcharo amesema Uharibifu wa mazingira ni kosa ambalo limekuwa likifanywa na binadamu, na kutoa wito kwa, wananchi  kujitahidi  kuendelea kuyaunza mazingira hayo ili yasiendelee kuharibiwa.


Amelipongeza shirika la UNDP kwa kuona umuhimu wa kuweza kuwasaidi fedha hizo kutokana na maeneo mengi ya wilaya ya Moshi kuharibiwa na wananchi wachache kwa manufaa yao binafsi.

Amesema changamato kubwa iliyopo kwa sasa ni kuendelea kuwaelimisha wananchi umuhimu wa  utunzaji bora wa mazingira na dhamana ya kuilinda misitu hiyo.


Aidha ameongeza kuwa TEACA, imeanza kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira, ambapo wameanza kwenye shuule za msingi na sekondari zilizopo katika wilaya ya Moshi.

No comments:

Post a Comment