Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Tuesday, November 4, 2014

Takribani vyama 48 vya msingi vya wakulima wa kawaha vyakosa mtaji wa kuingia kwenye mfumo wa uuzaji na ukusanyaji wa kahawa

KILIMANJARO zaidi ya vyama takribani 48 vya msingi  vya wakulima wa zao la kahawa  mkoani Kilimanjaro vimeshindwa kuingia katika mfumo mpya wa uuzaji na ukusanyaji wa zao hilo ulioletwa na serikali kutokana sababu mbalimbali ikiwemo  ukosefu wa mitaji.

Hayo yalibainishwa na Meneja Mkuu wa chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa zao hilo mkoani Kilimanjaro (KNCU) Onest Temba, wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana mjini moshi mkoani hapa.

Temba alisema kati ya vyama vya msingi 64 vya wakulima wa kahawa, vyama 9  ndivyo vilivyoweza kuanza kutumia mfumo mpya huku vingene 48 vikishindwa kusimama vyenyewe kutokana na ukosefu wa mitaji.

Aidha alisema ili kuvilinda vyama vilivyoshindwa visife na viendelee kufanya kazi KNCU itaendelea kuwa na vyama hivyo mpaka pale vitakapo kuwa na uwezo wa kusimama vyenyewe  na kujitegemea kufanya biashara hiyo kama  ilivyo kwa vyama vingine.

Alisema pamoja na vyama hivyo kuingia katika mfumo huo mpya bado vitaendelea kuleta ushuru KNCU na kwamba mfumo huo hauzuii KNCU kujikusanyia mapato yake kutoka katika vyama hivyo.

Kutokana na hali hiyo Meneja huyo aliwataka viongozi wa vyama hivyo kuwa makini kutokana na kwamba pasipo kuwa na utendaji na usimamizi mzuri kunauwezekanao mkubwa wa kuanguka kutokana na gharama za mikopo ya benki.

Alisema ni vema vya hivyo kuchukua mikopo kutoka benki kwaajili ya kufanya biashara hiyo na kuleta faida na kwamba kuchukua fedha na kuto timiza malengo waliyoyakusudia ni chanzo kikubwa cha kuporomoka kwa  vyama hivyo.

No comments:

Post a Comment