Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, July 8, 2015

HOSPITALI YA RUFAA YA KCMC YAFANYIWA MABORESHO


Hospitali ya rufaa ya KCMC iliyopo mkoani Kilimanjaro, inayomilikiwa kanisa la kiinjili la kiluteri Tanzania (KKKT) imeanza kufanyiwa upanuzi wa majengo yake ili kuondoa changamoto ya msongamano wa wagonjwa ambao umeongezeka kwa kiasi kikubwa kutokana na uchache wa majengo hususani kitengo cha upasuaji na kitengo cha dharura.

Kaimu mkurungenzi mkuu wa KCMC Profesa Raimos  Olomi, ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ambapo alisema upanuzi  huo utasaidia kuboresha zaidi huduma za kitabibu zitolewazo katika hospitali  hiyo, ambayo ina zaidi ya miaka arobaini tangu ilipojengwa.

Dokta  Giliarld  Masenga, ambaye ameteuliwa na bodi ya KCMC kushika nafasi ya mkurugenzi mkuu wa hospitali hiyo alisema kipaumbele chake ni kushawishi  uongozi wa hospitali kuongeza idadi ya watumishi ili kuondoa upungufu wa madaktari na wauguzi uliopo katika hospitali hiyo ambapo idadi ya wagonjwa imekuwa ikiongezeka kwa kiwango kikubwa.

No comments:

Post a Comment