Ferdinand
Shayo,Arusha.
Wakazi wa
kata ya Ungalimited mkoani Arusha
wameilalamikia serikali ya mtaa huo kwa kushindwa kudhibiti vitendo vya uporaji
vinavyofanyika katika maeneo yao hali inayoathiri shughuli za biashara na usalama wa mali zao.
Ni kufuatia
kukithiri kwa vitendo vya uporaji vinavyofanyika kwa uwazi hata nyakati za
mchana kwa wapita njia pembezoni mwa barabara ya Esso,Kona ya Nairobi ,Darajani
na mtaa wa Makaburi ya baniani.Kukosekana kwa udhibiti wa matukio ya uporaji
kumepelekea kushamiri kwa vitendo hivyo siku hadi siku.
Wakizungumza
kwa sharti la kutokutajwa majina yao kwenye gazeti,wakazi wa eneo hilo na
wafanyabiashara wameeleza kuwa viongozi wa mtaa wanayafahamu mambo hayo na
wamekuwa wakiyafumbia macho hawachukui hatua jambo linalosababisha kuonekana
kuwa wanakumbatia vitendo hivyo.
“Hakuna
mwizi anayeiba aliyetoka mbali na mtaa huo wezi wengi ni vijana ambao ni
wenyeji wa eneo hilo,wengine ni watoto wa viongozi wa mtaa,jambo hili linatukosesha
imani na viongozi wetu na kupelekea hisia kuwa wezi hao wanashirikiana na
viongozi kwasababu wezi wamekuwa wakikamatwa na kuachiwa bila kuchukuliwa hatua
za kisheria”
Wafanyabiashara
wa eneo hilo wamesema kuwa vitendo vya uporaji vimekuwa vikiathiri biashara zao
na kusababisha wateja kuwa wachache kwani vitendo hivyo vimekuwa vikiwatia hofu
,wamekuwa wakilazimika kuwahudumia wateja huku wakiwa makini kuwatahadharisha
wasikwapuliwe vitu vyao kama simu,mikoba,pamoja na mali zao.
Pia
wameeleza kutokuwa na imani na polisi jamii pamoja na Sungu sungu ambao baadhi
yao wanadaiwa kuhusika na vitendo vya uhalifu na wameiomba serikali ichukue
hatua madhubuti ya kudhibiti vitendo
hivyo ili kuhakikisha ulinzi na usalama katika maeneo yao.
Kwa upande
wake Mwenyekiti wa mtaa wa Makaburi ya Baniani Bwana Jumanne Abdallah amekanusha
madai ya wananchi hao na kusema
kuwa si ya kweli “Tunapowakamata wezi
tunachukua hatua za kuwahoji,kuwakutanisha na walalamikaji,kujiridhisha kuwa
tuhuma hizo ni za kweli kasha kuwafikisha
polisi.
“Tatizo mtu
anayeibiwa anapopatiwa vitu vyake kutoka kwa muhusika,ukimwambia amchukue
mtuhumiwa amchukulie hatua anakataa na kusema kuwa aoni haja ya kumpeleka
polisi wakati ameshapata vitu vyake kwasababu hana muda huo.Hili limekuwa likichochea vitendo hivi”
“Kwa eneo
langu lina polisi jamii vijana wasiopungua kuni (10) wanaosaidia kudhibiti
uhalifu mdogo mdogo mtaani kuanzia muda wa saa moja na nusu usiku,hili
limepunguza uporaji wa simu na mikoba kwa kiasi Fulani,changamoto tunayokabilana
nayo ni wananchi kuwa na mwitiko mdogo
wa kuchangia fedha kwa ajili ya kuwalipa posho vijana wanaojitolea kuwa polisi
jamii”
Bwana
Abdallah anaeleza changamoto nyingine ni walinzi kuwa wachache na wanaolindwa
kuwa wengi,unapolinda mwizi asiibe mwizi naye anakulinda kuwa unaelekea wapi
ili apate nafasi ya kuiba,Akijibu madai kuwa polisi jamii wa mtaa kudaiwa
kuhusika katika vitendo vya uporaji amekanusha pia madai hayo.
Ameeleza
kuwa vitendo hivyo vya uporaji vimekuwa vikichochewa na vijana wanaotumia madawa ya kulevya pamoja na
ukosefu wa ajira .Hivyo amewataka wananchi kuwa walinzi wa wenzao na
kushirikiana kutokomeza vitendo vya uhalifu.
No comments:
Post a Comment