Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, September 17, 2012

BWENI LA WANAFUNZI LAWAKA MOTO NJOMBE...!

Zaidi ya wanafunzi 93 wa kidato cha tatu na nne katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Wanike mkoani Njombe, wamenusurika kifo baada ya bweni lao kuteketea kwa moto.
 
Mkuu wa Wilaya ya Wang’ing’ombe, Esterina Kilasi, alisema tukio hilo lilitokea Septemba 13, mwaka huu saa 4:00 usiku.

Alisema moto huo uliteketeza vifaa mbalimbali  vya wanafunzi.

Hata hivyo, alisema moto huo hakuleta madhara kwa upande wa wanafunzi na thamani ya vifaa pamoja na chanzo cha moto huo havijafahamika.

CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment