Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, July 27, 2013

FAHAMU JINSI SIASA ILIYOTAWALA KWENYE MCHAKATO WA KATIBA MPYA ITAKAVYO WAUMIZA WATANZANIA

 MUDA mrefu nimekua nikijiuliza kwanini mchakato mzima wa ukusanyaji wa maoni kwa ajili ya katiba mpya ya Tanzania umekua na malumbano mengi sana na pia zaidi ya asilimia tisini ya kinachozungumzwa kwenye mchakato wa uundwaji wa katiba mpya ni maswala ya siasa tu. Lakini ukweli ni kwamba watanzania tulio wengi hatufahamu kuwa katiba ya nchi ndio muongozo mkubwa sana katika kuhakikisha wananchi wa Tanzania wanaishi kwa amani na pia wanazilinda rasilimali za nchi kwa kutegemea katiba ya nchi. Na sio kutumia asilimia zaidi ya tisini kujadili maswala ya siasa katika katiba maana mara nyingi mchakato wa kukusanya maoni kwa ajili ya katiba mpya unaonekana kuegemea sana upande wa siasa kuliko kulenga matatizo mengi yanayoikabili jamii. Kuna mambo ambayo kiukweli ukiyaangalia au kuyasikiliza utagundua kuwa watanzania wengi bado hatujafahamu umuhimu wa katiba na hata tunapopata nafasi ya kuchangia mawazo utakuta tunachangia masuala ya kisiasa tu.

 Kwa mfano unakuta kijana anapopewa nafasi ya kuchangia unamsikia akisema “Tunaomba katiba mpya itoe nafasi kwa mgombea binafsi” Na mtu huyo hana kazi ambayo inampatia kipato cha kumtosha kujikimu kwa maisha ya kawaida ya milo mitatu na kuishi kwenye nyumba yenye umeme na maji na uhakika wa matibabu. Nadhani lingekua jambo la busara kama kijana huyo angeweza kupendekeza katiba mpya itoe fursa kwa kila kijana anapo hitimu elimu awezeshwe kupata ajira au kupatiwa mkopo wenye masharti nafuu, au kuwe na sheria itakayowabana viongozi wa serikali kuweza kuiweka mikataba wazi hususani mikataba kati ya serikali na wawekezaji inayohusiana na rasilimali za nchi kama madini, mbuga za wanyama, gesi, na rasilimali nyingine nyingi.

Wakati mwingine unakuta mwanamke anapata nafasi ya kuchangia unamsikia akisema “Nafasi za wanawake ziongezwe bungeni ili kuweza kuleta usawa wa wanaume na wanawake bungeni au nafasi za viti maalumu vipewe kipao mbele kwa wanawake” Wakati mwanamke huyo elimu yake ni ya darasa la saba na hata uwezekano wa yeye kupata nafasi hiyo haupo kabisa na yeye mwenyewe anafahamu fika kuwa yeye hawezi kupata nafasi ya kwenda kuwakilisha bungeni. Nadhani ingekeua jambo la busara kama angetoa mchango kwa kuomba katiba mpya iweze kuondoa malipo kwa wakina mama wanapoenda kujifungua hospitalini, au katiba mpya pia itoe nafasi kwa wakina mama ambao wapo nyumbani wanalea familia waweze kuwa na mafao kutoka kwenye mshahara ambao waume zao wanalipwa ila kuwasaidia pale ambapo mume anapofukuzwa kazi, anapostaafu au anapo fariki.

Na mlemavu anapata nafasi ya kuchangia mchakato wa katiba mpya utamsikia anasema Serikali itukumbuke na sisi walemavu tupewe nafasi bungeni ili tuweze kutetea na kuzisimamia haki zetu na misaada inayotoka kwa nchi wahisani”  Wakati misaada ni mambo ambayo hayana uhakika na pia misaada haitolewi kila siku au kila wiki,  ila kuna maswala kama haki sawa katika sehemu za ajira, haki za kulindwa wakati wa machafuko ama vita maana walemavu ndio wahanga wakubwa sana wakati wa vita. Pia katiba mpya iweke bajeti kwa ajili ya kununua vifaa kwa ajili ya walemavu mashuleni na pia zijengwe shule maalumu za kutosha kwa ajili ya walemavu, tofauti na ilivyo sasa.

Mzee wa miaka zaidi ya hamsini anapata nafasi ya kuchangia katika uundwaji wa katiba mpya utamsikia anasema “Katiba mpya itoe nafasi ya wazee kuwa na bunge lake au wazee wapewe nafasi za viti maalumu bungeni”  Wakati hata wakipewa hizo nafasi bado zitakua ni chache sana na wala hazitaweza kukidhi matakwa ya wazee wote, wakati kuna maswala ambayo endapo yatapendekezwa kuweka kwenye katiba mpya yatawasaidia sana wazee kwa mfano  mafao ya uzeeni yaboreshwe na pia kwa wale wazee ambao hawakupata nafasi ya kuajiriwa nao wakifikizeeka pia walipwe ili kupunguza utegemezi na pia kuwanusuru wazee na vifo visivyo vya lazima kama kufa kwa njaa, kukosa matibabu, kuangukiwa na nyumba, n.k.

Hiyo ni mifano mchache tu lakini kuna mambo mengi sana ambayo yanatakiwa kuwepo kwenye katiba mpya na sio kuzungumzia siasa tuuu. Wakati wanasiasa nao wana nafasi zao za kuchangia kwenye mchakato wa katiba mpya.

By Joshua Fanuel
#teamKINGJOFA

No comments:

Post a Comment