Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, May 19, 2014

UGONJWA WA DENGUE TAYARI UMESHAFIKA MKOANI KILIMANJARO


KILIMANJARO Ugonjwa hatari wa dengue umedaiwa kuingia wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, ambapo watu wawili wamegundulika kuwa na dalili za ugonjwa huo, na hivyo wananchi  wa wilaya ya Hai wametahadharishwa kuwa makini  na kujikinga na mbu anayeeneza ugonjwa huo.

Tahadhari hiyo imetolewa na wataalumu wa afya wa wilaya ya Hai kufuatia kugunduliwa kwa watu wawili  wakiwa na dalili za ugonjwa wa Dengue ambao umekuwa tishio kubwa kwa wananchi wengi tangu ulipotangazwa kuingia nchini Tanzania na hususani katika mkoa wa Dar es salaam kuanzia mwanzoni mwa mwezi machi mwaka 2014.

Wakizungumza na waandishi wa habari  madaktari katika hospitali ya Wilaya ya Hai Dokta Julius Massawe  na Dokta  Happynes Ndenshau walisema mpaka sasa kuna dalili  za ugonjwa huo kuwepo wilaya Hai kutokana na watu  wawili kusadikiwa kuwa na dalili za ugonjwawa Dengue.

Dokta Julius Massawe amesema  watu hao wawili ambao wanasadikiwa kuwa walitokea jijini Dar es  Salaam  ambapo mmoja ni mkazi wa kijiji cha Narumu kata ya Narumu Mashariki na mmoja ni  mkazi wa mtaa wa Kibaoni katika wilaya ya Hai wanasadikika kuwa na dalili za ugonjwa huo ila madaktari hao wanasubiri vipimo zaidi kutoka
katika hospitali ya rufaa ya KCMC, ambapo wamepeleka damu ya watu hao kwa uchunguzi zaidi.

Dokta Massawe aliendelea kusema >> "kufuatia watu hao kuonesha dalili hizo za ugonjwa wa Dengue, ambao  kwa sasa wamelazwa katika hospiali ya St. Jose ya mjini Moshi wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari mapema pindi wanapohisi kuugua ugonjwa huo kwa kufika  katika hospitali ili waweze kupatiwa matibabu ya haraka."

Alifafanua kuwa wagonjwa hao wawili inasadikiwa kuwa walikuwa jijini Dar es Saalam kwa ajili ya kuwatembelea ndugu zao  na waliporejea nyumbani kwao walianza kuumwa na kugunduliwa kuwa wanadalili za ugonjwa huo hatari wa Dengue.

Dokta Ndenshau alisema >> "Wanachofanya kwa hivi sasa ni kutoa elimu kwa madaktari na wauguzi na watu wengine, ili wanapobaini mtu mwenye dalili za ugonjwa huo ni vizuri akapelekwa hospitali mapema."

Asema kwa sasa hakuna tiba wala chanjo ya ugonjwa huo, hivyo wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari dhidi ya maambukuzi  ya magonjwa yanayosababishwa na mbu.

Alizitaja dalili za ugonjwa huo kuwa ni kuumwa kichwa, homa kali, upungufu wa damu na kupoteza maji mwilini, hivyo wananchi wametakiwa kuwahi kituo cha afya mara moja pindi wanapohisi dalili kama hizo, au dalili kama za malaria.

No comments:

Post a Comment