MOSHI watu wawili wa familia moja ambao ni mke na mume wameuwawa kikatili na mtoto wao wa kiume kwa
kuwakatakata na kitu kilichosadikika kinaweza kuwa ni panga hadi ubongo kumwagika na kupelekea mauti kuwafika baada ya muda mfupi. Tukio hilo la kustaajabisha limetokea wilayani Hai mkoani
kilimanjaro.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa
Polisi mkoa wa Kilimanjaro Robert Boaz amewataja marehemu kuwa ni Shahidu Mohamed
Njau, miaka 60, na Minayi Mohamed Peter, miaka 57, wote wakazi wa kijiji cha Roo Kata ya
Masama Mashariki wilaya ya Hai.
Aliendelea kusema >> "Muuaji anajulikana kwa jina la Yusuph Shahidu Njau miaka 32 na taarifa za mwenyekiti wa serikali ya kijiji anasema
tukio hilo lilitokea tarehe 9 mwezi May 2014 saa 12 jioni."
Kamanda Boaz alisema >> "Mara baada ya kijana huyo kufanya tukio hilo, alichoma moto nyumba ya wazazi wake hao ambayo walikuwa wakiishi, ambapo majirani walifanikiwa kuzima moto huo kabla ya kuleta madhara makubwa."
Boaz alisema >> "Chanzo cha tukio hilo hakijajulikana na kwamba mtuhumiwa huyo mara baada ya kufanya tukio hilo alikimbia pasipo julikana."
Kamanda alisema >> "Jeshi la polisi, linaendela kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha tukio hilo pamoja na kumsaaka mtuhumiwa ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake."
Miili ya marehemu imehifadhiwa katika hosptali ya wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, ikisubiri taratibu za mazishi.
Kamanda Boaz alisema >> "Mara baada ya kijana huyo kufanya tukio hilo, alichoma moto nyumba ya wazazi wake hao ambayo walikuwa wakiishi, ambapo majirani walifanikiwa kuzima moto huo kabla ya kuleta madhara makubwa."
Boaz alisema >> "Chanzo cha tukio hilo hakijajulikana na kwamba mtuhumiwa huyo mara baada ya kufanya tukio hilo alikimbia pasipo julikana."
Kamanda alisema >> "Jeshi la polisi, linaendela kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha tukio hilo pamoja na kumsaaka mtuhumiwa ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake."
Miili ya marehemu imehifadhiwa katika hosptali ya wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, ikisubiri taratibu za mazishi.
Kwa upande wa mwenyekiti wa kijiji hicho
Alfan Mohamed alidhibitisha kutokea kwa tukio hilo na alisema >> "Baada ya kutoa msaada wa kuzima moto waliingia ndani na
kumkuta mama ameshafariki na baba mzazi akiwa mahututi na alipoteza maisha
akiwa njiani eneo la kwasadala akipelekwa hospitali."
No comments:
Post a Comment