Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, June 16, 2014

SERIKALI YAOMBWA KUTOA USHIRIKIANO KWA WASANII WA MKOA WA KILIMANJARO

KILIMANJARO serikali mkoani Kilimanjaro imeombwa kutoa ushirikiano kwa wasanii waliopo mkoani Kilimanjaro ili kuinua tasnia ya filamu mkoani Kilimanajro sanjari na kusaidia kukuza vipaji vya waigizaji na kushirikisha sanaa hiyo ambayo imeonekana ikipuuzwa mkoani Kilimanjaro.

Ombi hilo limetolewa na katibu wa chama cha waigizaji na wacheza picha jongefu mkoani Kilimanjaro, Ditram Ngonyani wakati wa mkutano mkuu wa kupitisha katiba ya chama hicho ambayo iliwashirikisha viongozi wa chama hicho kutoka katika wilaya zote za mkoani Kilimanjaro.

Ngonyani alisema mara nyingi wasanii wamekuwa wakikosa ushirikiano kutoka kwa viongozi wa serikali waliopo kwenye wilaya hususani maofisa utamaduni, jambo ambalo linazorotesha tasnia hiyo na kuiomba serikali kutoa ushirikiano ili kukuza utamaduni katika wilaya husika.

Amesema wakati mwingine maofisa utamaduni wamekuwa wakitoa kauli chafu kwa viongozi wa chama hicho kauli ambazo zimekuwa zikiwafanya kuonekana kutothaminiwa na serikali huku wengine wakipuuzwa pindi wanapoomba kukutana nao.

Katika hatua nyingine katibu huyo amewataka wasanii wanaoigiza kuvaa mavazi yenye heshima ili kuitangaza tasnia hiyo na kuacha kuvaa nusu uchi kutokana na hatua hiyo kuwa ni ya kidhalilishaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama hicho, Ramadhani Msasu, ameiomba serikali kupitia wizara ya habari, tamaduni na michezo kuacha kuwathamini wanamichezo wa mpira wa miguu zaidi na badala yake kutoa agizo kwa maofisa utamaduni wote kutoa ushirikiano kwa vyama vya sanaa kwani wao ndiyo wanaotangaza utamaduni wa mtanzania.

No comments:

Post a Comment