THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O.
BOX 9120,
DAR
ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za pole Rais wa Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein
kufuatia kuuawa kwa mtu mmoja na wengine sita kujeruhiwa akiwemo mhubiri
wa amani ajulikanaye kama Sheikh Ahmed Haidari Jabir wa Zanzibar, kutokana na
kurushwa kwa Bomu katika shughuli ya
kidini iliyokuwa ikifanyika katika eneo la Darajani tarehe 13 Juni,2014, mjini Unguja.
‘Hicho
ni kitendo cha kulaaniwa kwa nguvu zote na watu wote wapenda amani Bara na
Visiwani, ni kitendo cha woga na kisicho na ustaarabu na wala hakikubaliki
katika dunia ya sasa’ Rais amesema na kuongeza kuwa;
‘Hiki
ni kitendo kilichofanywa na watu waoga, wasio na ustaarabu wa aina yeyote ile’.
Rais amekemea na kuwataka watu kuwa wastaarabu, wavumilivu na kuheshimu imani
na mitizamo ya watu wengine hata kama hawakubaliani nao.
Rais
amesema amesikitishwa zaidi na watu hao wasio na ustaarabu ambao wamefanya
kitendo hicho cha kihalifu kwenye shughuli ya kidini ambapo ndipo mahali
panapostahili Amani, Uvumilivu na Unyenyekevu zaidi kwa kuwa ni wakati ambapo
binadamu anapofanya mawasiliano na muumba wake.
Rais
Kikwete amelitaka Jeshi la Polisi kuwasaka na kuwafikisha mbele ya vyombo vya
haki wale wote waliohusika katika tukio hilo lisilo la kistaarabu.
Imetolewa
na;
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu-Dodoma
15 Juni, 2014
No comments:
Post a Comment