Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, June 18, 2014

Watuhumiwa Wa Mauaji Mpeketoni Wakamatwa

Photo: Kwa nini Mpeketoni ilishambuliwa?
Saa nne unusu jioni Jumapili, Ufaransa ilikuwa inacheza dhidi ya Honduras katika mojawapo ya mechi za kombe la dunia.

Lakini mechi ilipokuwa inaendelea,katika eneo la Mpeketoni mauaji ya kinyama yalikuwa yakifanyika.
Ujumbe kutoka kwa afisa mmoja wa shirika la msalaba mwekundu ulikuwa na ishara zote za mashambulizi ya kigaidi sawa na kile ambacho wengi wamekuwa wakishuhudia katika mbinu ya mashambulizi inayotumika na Boko Haram nchini Nigeria.

''Milio mikubwa ya risasi inasisika katika eneo la Mpeketoni, katika jimbo la Lamu. Mashambulizi yamekuwa yakiendelea kwa saa moja sasa. Kituo cha petroli kimeteketezwa na hoteli kushambiliwa.Tunasubiri taarifa zaidi,'' alisema afisaa huyo wa shirika la Red Cross.

Usiku wa kuogofya wenye mashambulizi ambayo yalidumu kwa muda wa saa kumi. Walioshuhudia walisema waliona zaidi ya watu 50 wakiwa wamejihami vikali na kuanza kufanya msako ndani ya nyumba za watu.

Magari mawili yaliyokuwa yameibwa ndiyo yaliyotumika kuwabeba washambulizi hadi katika eneo la Mpeketoni umbali wa kilomita 40 kutoka ufuo wa bahari hindi.

Mashambulizi hayakuharakishwa. Washambuliaji walisemekana kuongea Kisomali na kiswahili huku wakibeba bendera ya Al Shabaab na kutamka 'Allahu Akbar'', yaani Mungu ni mkubwa.

'Kwa nini Mpeketoni? '
Eneo hilo ambalo halina ulinzi mkali bila shaka lilikuwa sehemu ya karibu sana kwa Al Shabaab kushambulia. Linakaribiana na Somalia. Kundi hilo halikusita kukikri kutekeleza mashambulizi hayo, saa 24 baadaye.

Walioshuhudia walisimulia visa vya kuogofya wakati washambuliaji walipokuwa wanaendesha mashambulizi nyumba hadi nyumba wakimuua kila mwanamume waliyemuona 

anawake na watoto walisazwa. Mashambulizi yalifanya kwa masaa kadhaa kabla ya polisi kuchukua hatua.

Mfumo wa mashambulizi na ukubwa wa mashambulizi yenyewe umewaacha wengi wakiwa na maswali si haba. Kwa nini Mpeketoni? Na kwa nini wanaume pekee ndio waliouwa?

Al Shabaab walituhumiwa kwa mauaji ya wanawake na watoto katika shambulizi la awali dhidi ya jengo la kifahari la Westgate mwaka jana mjini Nairobi.

Mashambulizi ya kiholela ambayo pia yaliwalenga waisilamu, yaliwaghadhabisha wale ambao huunga mkono kundi hilo.

'Al Shabaab wabadili mbinu'

Al Shabaab sasa wameamua kubadili mbinu wanaotumia kushambulia kwa hofu ya kupoteza uungwaji mkono

Shambulizi la Mpeketoni, ilikuwa njia mojawapo ya kusafi sifa yao. Kuua wanaume na kuwasaza wanawake na watoto.

Mpeketoni ni eneo lenye rotuba nzuri ya kufanyia kilimo wala sio eneo ambalo ni kivutio kwa watalii. Maafisa wa usalama huenda walikutwa ghafla bila ya kujiandaa kukabiliana na shambulizi la aina yoyote.
Katika siku za nyuma, makundi ya kigaidi yamekuwa yakilenga miji mikubwa ya Kenya kwa mashambulizi lakini sasa inaonekana kuwa kundi hilo limeanza kubadili mbinu ya mashambulizi na kuanza kulenga vijiji.

Serikali ya Kenya imelaumu uchochezi wa kisiasa kwa mashambulizi hayo na kuwaonya wanasiasa dhidi ya kuchochea ghasia na matamshi ya chuki miongoni mwa wananchi.

Kuna mjadala mkali kuhusu nani aliyetekeleza mashambulizi hayo. Baadhi wanahisi kuwa licha ya kwamba Al Shabaab wamekiri kuyatekeleza, sio wao , serikali ya Kenya imesema wazi kuwa yalichochewa kisiasa.

Source: bbc.co.uk
Source: bbc.co.uk

Polisi nchini Kenya wamesema kuwa wamewakamata washukiwa wawili wa mashambulizi yaliyofanyika mjini Mpeketoni, Pwani ya Kenya na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 60.

Kundi la wapiganaji wa Al Shabaab limekiri kufanya mashambulizi hayo yaliyofanyika Jumapili usiki na Jumatatu usiku ingawa serikali ya Kenya imesema kuwa mashambulizi hayo yalichochewa kisiasa.

''Tumewakamata watu kadhaa kuhusiana na mashambulizi ya Mpeketoni, akiwemo miliki wa gari moja lililotumika katika mashambulizi hayo,'' alinukuliwa akisema mkuu wa polisi David Kimaiyo.

Mshukiwa wa pili aliyekuwa anaandika kwenye akaunti ya Twitter inayoshukiwa kumilikiwa na Al Shabaab pia alikamatwa. Anadaiwa kutangaza kuwa Al Shabaab ndio waliofanya mashambulizi hayo

Licha ya madai ya haraka kutoka kwa kundi la Al Shabaab kuwa wao ndio waliotekeleza mashmabulizi hayo, Rais Uhuru Kenyatta katika hotuba yake kwa taifa alilaumu vikundi vya wanasiasa pamoja na makundi ya watu ambayo yana nia ya kufaidi kutokana na hali mbaya ya usalama nchini humo kwa kufanya mashambulizi hayo.

Maafisa kadhaa wa polisi wa eneo la Mpeketoni, wamefutwa kazi na wengine kuhamishwa kutoka vituo vyao vya kazi katika eneo hilo.

Hii ni baada ya tuhuma dhidi yao kuwa walipuuza onyo la kutokea kwa mashambulizi hayo kutoka kwa shirika la ujasusi. Wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka.

Source: bbc

No comments:

Post a Comment