Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Tuesday, July 8, 2014

BAADHI YA PICHA NA MAELEZO YA BOMU LILILORUSHWA KATIKA MGAWAWA JIJINI ARUSHA

  Askari wa Jeshi la Wananchi JWTZ kitengo cha Mabomu wakiwa katika eneo la tukio ambapo bomu lilirushwa ndani ya Mgahawa ujulikanao kwa jina la Traditional Indian Cusine uliopo pembeni ya hotel ya Gymkana jijini Arusha.
 
  Majeruhi wa mlipuko wa bomu uliotokea katika mgahawa wa Traditional Indian Cusine aliyejulikana kwa jina la Deepak Gupta (25), akiwa amelazwa katika hospitali ya Selian, katika chumba cha watu mahututi (ICU), mara baada ya kukatwa mguu wake mmoja wa kushoto kutokana na mguu huo kujeruhiwa vibaya na bomu.
 
 Sehemu ya baadhi ya watu waliojeruhiwa kwenye mlipuko wa bomu uliotokea jana usiku katika mgahawa wa Traditional Indian Cusine wakiwa wamelazwa katika hospitali ya Selian, jijini Arusha kwa matibabu.
 
  Uharibifu uliofanywa na bomu hilo.

 Watu wanane wamejeruhiwa usiku wa kuamkia leo baada kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu kurushwa katika mgahawa ujulikanao kama Vama uliopo katika jengo la club ya gymkhana karibu na mahakama kuu ya mkoa wa Arusha.

Katika tukio hilo lililotokea majira ya saa 4.30 usiku baada ya watu wasijulikana wanaodaiwa kurusha kitu hicho kilichosababisha mlipuko mkubwa ambao ulijeruhi baadhi ya wateja waliokuwepo katika mgahawa huo ambapo majeruhi hao walikimbizwa katika hospitali ya seliani ya mjini Arusha.

Kaimu mkurugenzi  mkuu wa hospitali ya seliani dr.Paul Kisanga amethibitisha kupokea majeruhi 8  kati yao wamo  wanaume watano na wanawake 3 wakiwemo watoto wawili wote raia wa Tanzania wenye asili ya Asia huku akimtaja Deepack Gapla kuwa na hali mbaya ikiwa ni pamoja na kupoteza mguu mmoja na hivi sasa yupo chini ya uangalizi maalum ICU.

Camera yetu ilifika katika eneo la tukio na kukuta eneo hilo likiwa chini ya uangalizi maalum wa askari jeshi la wananchi kitengo maalum cha uchunguzi wa mabomu kwa kushirikiana na jeshi la polisi wakiendelea na uchunguzi wa chanzo cha mlipuko huo ambapo waandishi wa habari walipojaribu kuwasiliana na kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas alikataa kuzungumzia suala hilo kwa madai kuwa suala hilo litatolewa ufafanuzi makao makuu ya jeshi na mkurugenzi wa upelelezi makosa ya jinai DCI Isaya Mghulu.
 
 Picha kwa hisani ya Jiachie Blog.

No comments:

Post a Comment