WAKAZI wa mkoa wa Kilimanjaro, hususani wagonjwa, wameondokana na adha ambayo walikuwa wakiipata wakati walipokuwa wakifika katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa kilimanjaro Mawenzi kwa ajili ya matibabu, baada ya Hospitali hiyo kupatiwa msaada wa mashine ya (Ultra sound).
Wakizungumza wananchi hao, Mariam Mauld na Michael Mauki wamesema, wagonjwa wengi ambao walikuwa wakifika katika hospitali hiyo walishindwa kufanyiwa uchunguzi kutokana na mashine hiyo kutokuwepo.
Mauki ambaye ni mkazi wa kata ya Rau alisema, aliwahi kufika katika hospitali hiyo kwa lengo la kupima magonjwa ya Figo, lakini alishindwa kuhudumiwa kutokana na kutokuwepo kwa kipimo hicho, na kwamba kuwepo kwa mashine hiyo itasaidia kuokoa maisha ya wagonjwa wengi wakiwemo wa mama wajawazito.
Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo, Mganga mfawithi wa hospitali ya Mawenzi, Dkt. Lwezaura Fredrick, alisema kwa takribani mwaka mmoja na nusu hospitali hiyo ilikuwa haina kifaa hicho hivyo wagonjwa walikuwa wakilazimika kwenda katika hospitali za binafsi na ya rufaa KCMC kwa ajili ya uchunguzi.
Alisema "akina Mama wajawazito ambao walikuwa wakifika hapa kwa ajili ya kupima walikuwa wakipata changamoto kubwa ya ukosefu wa kifaa hicho, na kwamba tatizo hilo limepatiwa ufumbuzi baada ya benki ya KCB ya mjini Moshi, kutoa msaada huo wenye thamani ya Shilingi milioni 15. lengo likiwa ni kutatua adha waliyukuwa wakiipata wagonjwa hao."
Amesema wagonjwa wengi walikuwa wakilazimika kwenda katika hospitali binafsi na kutibiwa kwa garama kubwa, na kwamba kuwepo kwa kuwepo kwa mashine hiyo katika hospitali hii itatatua changamoto hizo.
Awali akikabithi mashine ya ultra saund meneja wa benki ya KCB Moshi, Oforo Erasmo, amewaomba kuitumia mashine hiyo vizuri na kuitunza ili idumu pamoja na kuwasaidia wagonjwa wengi wa mjini Moshi.
Erasmo alisema kwa mwaka huu KCB imetenga jumla ya Shilingi milioni 350, kwa ajili ya kuhudumia jamii nchi nzima, katika nyanja za kielimu, Afya, Maji na Mazingira.
Naye kaimu katibu tawala mkoa wa kilimanjaro Mhandisi, Alfred Shayo, amepongeza benki ya KCB kwa msaada waliotoa hali ambayo itasaidia kuboresha afya za wagonjwa.
Wakizungumza wananchi hao, Mariam Mauld na Michael Mauki wamesema, wagonjwa wengi ambao walikuwa wakifika katika hospitali hiyo walishindwa kufanyiwa uchunguzi kutokana na mashine hiyo kutokuwepo.
Mauki ambaye ni mkazi wa kata ya Rau alisema, aliwahi kufika katika hospitali hiyo kwa lengo la kupima magonjwa ya Figo, lakini alishindwa kuhudumiwa kutokana na kutokuwepo kwa kipimo hicho, na kwamba kuwepo kwa mashine hiyo itasaidia kuokoa maisha ya wagonjwa wengi wakiwemo wa mama wajawazito.
Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo, Mganga mfawithi wa hospitali ya Mawenzi, Dkt. Lwezaura Fredrick, alisema kwa takribani mwaka mmoja na nusu hospitali hiyo ilikuwa haina kifaa hicho hivyo wagonjwa walikuwa wakilazimika kwenda katika hospitali za binafsi na ya rufaa KCMC kwa ajili ya uchunguzi.
Alisema "akina Mama wajawazito ambao walikuwa wakifika hapa kwa ajili ya kupima walikuwa wakipata changamoto kubwa ya ukosefu wa kifaa hicho, na kwamba tatizo hilo limepatiwa ufumbuzi baada ya benki ya KCB ya mjini Moshi, kutoa msaada huo wenye thamani ya Shilingi milioni 15. lengo likiwa ni kutatua adha waliyukuwa wakiipata wagonjwa hao."
Amesema wagonjwa wengi walikuwa wakilazimika kwenda katika hospitali binafsi na kutibiwa kwa garama kubwa, na kwamba kuwepo kwa kuwepo kwa mashine hiyo katika hospitali hii itatatua changamoto hizo.
Awali akikabithi mashine ya ultra saund meneja wa benki ya KCB Moshi, Oforo Erasmo, amewaomba kuitumia mashine hiyo vizuri na kuitunza ili idumu pamoja na kuwasaidia wagonjwa wengi wa mjini Moshi.
Erasmo alisema kwa mwaka huu KCB imetenga jumla ya Shilingi milioni 350, kwa ajili ya kuhudumia jamii nchi nzima, katika nyanja za kielimu, Afya, Maji na Mazingira.
Naye kaimu katibu tawala mkoa wa kilimanjaro Mhandisi, Alfred Shayo, amepongeza benki ya KCB kwa msaada waliotoa hali ambayo itasaidia kuboresha afya za wagonjwa.
No comments:
Post a Comment