THE
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S OFFICE,
STATE
HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete amewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya kote nchini
kuhakikisha kuwa wanashirikiana na Wananchi kuhakikisha kuwa ifikapo Mwezi
Novemba Mwaka huu, kila Shule ya Sekondari katika maeneo yao, ina
maabara kwa ajili ya masomo ya Sayansi.
Rais
Kikwete amesema hayo Mkoani Tanga katika nyakati tofauti Wilayani Kilindi na
Lushoto ambapo yuko katika ziara ya kikazi Mkoani Tanga tangu tarehe 8 Julai
hadi tarehe 12 Julai,2014.
"Nataka
ifikapo Mwezi Novemba, Mwaka huu vyumba vya maabara viwe vimekamilika,
tulipeana miaka miwili, imetimia" Rais amesema na kuongeza
kuwa lazima tusahihishe makosa tuliyofanywa ya kutojenga maabara wakati
tunajenga shule za sekondari nchini kote.
Mwaka
2006, Serikali ilihamasisha ujenzi wa Shule za Sekondari nchini kote na
muitikio ni mzuri, lakini hakukuwa na uhamasishaji wa kujenga maabara. “Tumeamua
kushughulikia suala la maabara ili kuongeza idadi ya wanafunzi wa masomo ya
Sayansi kote nchini." Rais amesisitiza.
Rais
amesema ameridhika na upanuzi wa Elimu katika ngazi za Msingi na Sekondari kote
nchini na Serikali inaendelea na hatua ya kutatua changamoto za ubora wa Elimu,
kuongeza Walimu, kuongeza Vitabu, ujenzi wa Maabara na Nyumba za Walimu kote
nchini.
Akihutubia
katika mkutano wa hadhara Wilayani Lushoto Rais ameahidi kuboresha na
kushughulikia suala la ujenzi wa barabara ya kwenda Bumbuli na zaidi
kuhakikisha anaweka barabara ya lami katika mji wa Lushoto na mji mdogo wa
Bumbuli.
Rais
anaendelea na ziara Wilayani Lushoto na Mkinga ambapo anaendelea kuzindua
miradi na kukagua miradi ya maendeleo.
Imetolewa na;
Premi
Kibanga,
Mwandishi
wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu – Dar es Salaam.
10
Julai,2014
No comments:
Post a Comment