Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Sunday, July 6, 2014

KANISA LA KKKT KUJENGA MAKAO MAKUU YA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA ASKOFU STEFANO

KILIMANJARO kanisa la KKKT dayosisiya kaskazini  limeanzisha mradi wa upatikanaji wa nishati inaotokana na kinyesi cha ng’ombe  kwajili ya matumizi mbalimbali hususani ya kupikia mradi  ambao utasaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa  tatizo la uharibifiu wa mazingira ususani ukataji wa miti .
Mradi huo umeanzishwa na KKKT kwa  ushirikiano wa Tanzania domestic program kupitia taasisi ya camatec ambapo wametoa elimu kwa wananchi kuachana na  matumizi ya nishati itokanayo na miti na badala yake watumie nishati itokanayo na kinyesi cha ng’ombe yaani (biogas), na tayari mitambo 150 imeshajengwa katika wilaya 5 za mkoa wa Kilimanjaro.
Kauli hiyo imetolewa na Askofu mkuu wa KKKT wa dayosisi hiyo Dr. Martin Shao, Wakati akizindua siku ya upandaji miti katika kijiji cha nshara wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, kwenye  eneo linalo tarajiwa kujengwa machame kampasi ya chuo kikuu cha kumbukumbu ya Askofu Stefano kinachomilikiwa na kanisa la KKKT.
Aidha Askofu Shayo amevipongeza vijiji  vya  uronu, nshara na ufoo, kwa kulipatia kanisa hilo eneo lenye ukubwa wa hekati 50 za ardhi kwaajili ya kujenga makao makuu ya chuo hicho ambapo katika uzinduzi huo, baadhi ya waumini wa kanisa hilo waliotesha miti kuzunguka katika eneo hilo.
Mkuu wa chuo hicho  Anold Temu amesema wakati mchakato wa ujenzi huo ukiendelea chuo kitaanza kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa waalimu wa shule mbalimbali za sekondari na baada ya ujenzi kukamilika, kitatoa masomo ya shahada ya sayansi kwa wanafunzi na waalimu hapa nchini na mataifa mbalimbali Duniani.

No comments:

Post a Comment