Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, July 3, 2014

MKURUGENZI WA MANISPAA APEWA MIEZI MINNE KUWAPATIA WAFANYABIASHARA ENEO LA KUDUMU

KILIMANJARO serikali mkoani Kilimanjaro imempa miezi minne Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Shaaban Ntarambe, awe ametoa maamuzi juu ya hatima ya wafanyabiashara wa soko la mitumba la Memorial kupatiwa eneo la soko ambalo litakuwa la kudumu kuliko ilivyo sasa.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu  wa mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama wakati alipokuwa akiongea na wafanyabiashara wa soko hilo katika mkutano uliowashirikisha wafanya biashara na wananchi wa kata ya Soweto, ambapo mkuu mkoa huyo amewataka wafanyabiashara hao kufanya biashara zao kwa uhuru bila ya mtu wa kuja na kuwabughudhi hadi hapo Manispaa itakapo wapatia eneo la kudumu.

Gama ametoa miezi minne kwa Manispaa wawe wametoa tamko la hatima ya wafanyabiashara wa soko la Memorial kupatiwa eneo ambalo litakuwa la kudumu kuliko ilivyo sasa, na kwamba amepiga  marufuku Manispaa kwenda na kuwaondoa wafanyabiashara hao bila ya kuwapatia eneo ambalo litakuwa la kudumu katika kufanyia biashara zao,.

Ameema  wapo watu wamekuwa wakilichukulia soko hilo kuwa kama  medali za siasa katika kuwatishia wafanyabisahara hao kuwa watakuja kuondolewa na kuwataka wasikubali kuondolewa hadi hapo Manispaa itakapo wapatia eneo la kufanyia biashara hizo.

Amesema Uchumi wa mkoa wa Kilimanjaro unategemea sana masoko kama haya, hivyo sitaki kusikia ugomvi unatokea katika soko hili, kuna watu wachache wamekuwa wakitumia Mamlaka yao kwenda kuwakamata na kuwanyang’anya  bidhaa zao , hili sitaki kulisikia katika mkoa wangu likijitokeza.

Aidha ameongeza kuwa ni vyema Manispaa wakaharakisha mchakato wa upatikanaji wa eneo hilo ili wafanyabiashara hao wafanye kazi ambazo zitakuwa rasmi na kuwepo kwa miundombinu itakayo wezesha upatikanaji wa huduma zote.

No comments:

Post a Comment