Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, July 3, 2014

WANANCHI WA PASUA WAMTUHUMU DIWANI WAO KWA KUJIMILIKISHA ENEO LA WAZI

Wakazi wa kata ya Pasua katika manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro wanamlalamikia diwani wa kata hiyo Charles Mkarakara kwa kujimilikisha  eneo la wazi  lililotengwa  kwaajili ya shughuli maalumu katika kata hiyo.

Malalamiko hayo yametolewa na wakazi  hao kwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama, mda mchache baada ya kuweka jiwe la msingi la bweni la wavulana wa shule ya sekondari ya Anna Mkapa, lililopo katika manispaa ya Moshi  mkoani kilimanjaro.

Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya wakazi hao Loti Martin na Dastan Biru  walimwambia   mkuu wa mkoa kuwa, wanasikitika kwa kitendo cha  diwani wao kupora  eneo ambalo lilitengwa kwajili  ya kituo cha mabasi, na badala yake amebadili matumizi na kujimilikisha eneo hilo na tayari ameanza maandalizi ya ujenzi .   

Kufuatia hali hiyo, mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonodas Gama amemwagiza afisa mipango miji wa manispa ya Moshi  Alex Poteka na mkuu wa wilaya ya Moshi Ibrahimu Msengi kusimamisha ujenzi usiendelee katika eneo hilo kisha paitishwe kikao cha kamati ya maendeleo ya kata (ward c) ili kupata ufafanuzi wa jambo hilo.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Pasua Charles Mkarakara, ambye pia ni mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya kata hiyo, amekiri kulifahamu eneo hilo na kufafanua kuwa  eneo hilo ni mali yake analolimiliki  kihalali .
 

No comments:

Post a Comment