MWENYEKITI wa halmashauri ya wilaya ya kilosa mheshimiwa Ameir Mubaruk
amewaagiza viongozi wa vijiji na kata ya Lumuma iliyopo wilayani Kilosa
kuhakikisha katika kipindi hiki cha kiangazi wanawaondoa wafugaji wote wavamizi
waliovamia katika maeneo ya wakulima.
Kauli hiyo imetolewa na Mheshimiwa
Mubaruk wakati akizungumza na wananchi wa kitongoji cha Manyomvi
kilichopo kata ya lumuma wilayani kilosa katika sherehe ya siku ya mkulima
iliyoandaliwa na mradi wa mpango wa kupunguza hewa ukaa inayotokana na
uharibifu na ufyekaji ovyo wa misitu MKUHUMI uliopo chini ya shirika la
kuifadhi misitu ya asili Tanzania TFCG.
Kwa upande wake afisa kilimo wa
mradi wa mkuhumi bwana shadrack yoash nyungwa…..ameelezea lengo la kuadhimisha
sherehe hiyo ya siku ya mkulima kuwa ni kupongezana na kupeana zawadi kwa
mkulima aliyefanya vizuri shambani kwake sambamba na kupeana zawadi ili iwe
chachu kwa wakulima wengine kuongeza juhudi katika kipindi kijacho cha kilimo
na kutimiza lengo la mradi la kutoa elimu hiyo.
No comments:
Post a Comment