MOSHI serikali kupitia wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
imesema itaendelea kuviboresha vyuo vyote vinavyofundisha wauguzi hapa nchi ili kuwa na uwezo mkubwa wa kuchukua wanafunzi wengi kuliko ilivyo sasa.
Hayo yamesemwa na waziri wa Afya, Dkt Seif Mohamed Rashid, wakati alipokuwa akikabidhi vitanda 18, magodoro pamoja na Mashuka 90 kwa halmashauri ya Same, ajili ya wodi za wamama wajawazito, wa kata 16 za jimbo la same
Mashariki, halfa ambayo iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Same, mkoani Kilimanjaro.
Waziri huyo, amesema mkakati uliopo kwa sasa katika wizara yake ni kuviboresha vyuo hivyo ili kuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi wengi kuliko ilivyoa sasa ambapo vyuo hivyo vinachukuwa wanafunzi 40 hadi 50, kwa mwaka na kwamba kuboreshwa kwa vituo hivyo vitaweza kuchukua wanafunzi 400 kwa mwaka.
Amema huduma za afya kwa ujumla wake bado zina gharama kubwa, na kwamba kwa nchi ya Tanzania wastani wa mtu mmoja anatumia kiwango cha dola 41, za kimarekani kwa mwaka kujitibu, ambapo kwa marekani wanatumia wastani wa kila mtu mmoja dola 6,000 hadi 9000, kwa mwaka, na kuwaomba wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya afya ambao utaweza kupunguza matatizo yanayowakabili.
Awali Meneja wa NMB kanda ya Kaskazini, Vick Bishubo, amesema wametoa msaada wa Vitanda, Mashuka na Magodoro, vikiwa na jumla ya shilingi milioni 15, ili kuweza kuokoa maisha ya wa Mama ambao walikuwa wakijifungulia chini.
Amesema sekta ya afya imekuwa ikikabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa vitanda vya kujifungulia katika vituo vya afya na zahanati, hivyo Benki ya NMB, imetenga jumla ya shilingi bilioni 1.3 kwa mwaka 2014 ili kusaidia jamii katika Nyanja ya Elimu, afya na Michezo.
Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Same Mashariki, Anna kilango, licha ya kuipongeza Benki ya MNB, kwa kutoa msaada huo, ambao utapungua adha ya wajawazito kujifungulia majumbani, pia ameiomba serikali kuwapatia watumishi wa afya ili waweze kutoa huduma iliyo bora.
Hayo yamesemwa na waziri wa Afya, Dkt Seif Mohamed Rashid, wakati alipokuwa akikabidhi vitanda 18, magodoro pamoja na Mashuka 90 kwa halmashauri ya Same, ajili ya wodi za wamama wajawazito, wa kata 16 za jimbo la same
Mashariki, halfa ambayo iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Same, mkoani Kilimanjaro.
Waziri huyo, amesema mkakati uliopo kwa sasa katika wizara yake ni kuviboresha vyuo hivyo ili kuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi wengi kuliko ilivyoa sasa ambapo vyuo hivyo vinachukuwa wanafunzi 40 hadi 50, kwa mwaka na kwamba kuboreshwa kwa vituo hivyo vitaweza kuchukua wanafunzi 400 kwa mwaka.
Amema huduma za afya kwa ujumla wake bado zina gharama kubwa, na kwamba kwa nchi ya Tanzania wastani wa mtu mmoja anatumia kiwango cha dola 41, za kimarekani kwa mwaka kujitibu, ambapo kwa marekani wanatumia wastani wa kila mtu mmoja dola 6,000 hadi 9000, kwa mwaka, na kuwaomba wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya afya ambao utaweza kupunguza matatizo yanayowakabili.
Awali Meneja wa NMB kanda ya Kaskazini, Vick Bishubo, amesema wametoa msaada wa Vitanda, Mashuka na Magodoro, vikiwa na jumla ya shilingi milioni 15, ili kuweza kuokoa maisha ya wa Mama ambao walikuwa wakijifungulia chini.
Amesema sekta ya afya imekuwa ikikabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa vitanda vya kujifungulia katika vituo vya afya na zahanati, hivyo Benki ya NMB, imetenga jumla ya shilingi bilioni 1.3 kwa mwaka 2014 ili kusaidia jamii katika Nyanja ya Elimu, afya na Michezo.
Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Same Mashariki, Anna kilango, licha ya kuipongeza Benki ya MNB, kwa kutoa msaada huo, ambao utapungua adha ya wajawazito kujifungulia majumbani, pia ameiomba serikali kuwapatia watumishi wa afya ili waweze kutoa huduma iliyo bora.
No comments:
Post a Comment