Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Sunday, July 6, 2014

VIJANA WATAKIWA KUWA NA UJASIRI WA KUTUMIA VYEMA FURSA ZINAZOTOLEWA

Vijana wanaopitia vyuo vya elimu ya juu hapa nchini wametakiwa kuwa na ujasiri na kutumia vyema fursa zinazotolewa na Diplomasia ya Uchumi, katika kukabiliana na changamoto za ajira.

Wito huo umetolewa jijini Dar es salaam na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka wakati alipokuwa akizungumza kwenye kongamano la vijana wa elimu ya juu kuhusu kukuza Diplomasia ya Uchumi.

Prof. Tibaijuka amebainisha kwamba vijana wa Kitanzania wanaweza kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira kupitia uhusiano na ushirikiano na vijana wenzao kutoka mataifa mengine.

Kongamano hilo limeandaliwa na Chama cha Mapinduzi Mkoa Maalumu wa vyuo vya Elimu ya Juu ambapo wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali vya elimu ya juu wameshiriki.

No comments:

Post a Comment