Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Sunday, July 6, 2014

WANANCHI WASHAURIWA KULITUMIA DAWATI LA JINSIA ILI KUINUSURU JAMII NA UKATILI WA KIJINSIA

HANDENI wananchi wilayani Handeni mkoani Tanga wameshauriwa kulitumia dawati la jinsia lililopo katika idara ya polisi kuelezea matatizo yanayowakabili bila woga ili kuweza kupunguza masuala ya unyanyasaji yanayoendelea kujitokeza kila siku katika jamii.

Kamanda wa polisi wilaya ya Handeni Zuberi Chembera alisema hayo ofisini kwake juzi alipokuwa akiongea na mtandao huu na kusema kuwa wananchi wasiogope kwenda polisi kwani kuna dawati hilo la jinsia na kazi yake ni kuwasikiliza na kuwasaidia matatizo yanayowakabili.

Alisema dawati hilo kwa kushirikiana na idara nzima ya polisi, kamati ya ulinzi na usalama na idara za elimu zimejitahidi kutoa elimu kwa wazazi, wanafunzi na walezi kuhusu umuhimu wa elimu kwa watoto wao ambapo takwimu zinaonesha kuwa wameitikia wito na kwasasa kiwango cha wanafunzi wanaopata mimba wilayani Handeni kimepungua.

Kamanda Chembera alisema mwaka jana 2013 mwezi Januari hadi mwezi Mei takwimu zinaonesha kuwa wanafunzi 22 walipata ujauzito hali iliyosababisha wanafunzi hao kushindwa kuendelea na masomo, kitu ambacho kimekuwa kikididimiza taaluma yao ila kwa takwimu za mwaka huu 2014 mwezi Januari mpaka mwezi Mei zinaonesha ni wanafunzi sita tu  ndio wameripotiwa katika dawati hilo kuwa na ujauzito na kesi zao zimeshaanza kufanyiwa kazi.

Alisema mwaka jana 2013 mwezi Januari hadi mwezi Mei kulikuwa na kesi 38 zinazohusu masula ya mimba kwa wanafunzi ambayo ni idadi kubwa sana kwao lakini mwaka huu zimepungua hadi kufikia 27 hali ambayo inadhihirisha kuwa elimu inayotolewa kwa wahusika imeeleweka na watoto wanaweza kufanya vizuri.

“Mwaka jana 2013 hadi mwezi Julai tayari zilisharipotiwa kesi za mimba 22 na kufunguliwa mahakamani kesi 38 lakini tunaona kuwa kuna mafanikio kwa elimu tunazotoa kwa wahusika kuhusu umuhimu wa elimu kwa watoto wetu kwani takwimu hizo zimepungua na hadi sasa kesi za mimba zilizopo ni 6 tu kutoka 22 na zilizopo mahakamani ni 27 kutoka 38 za mwaka jana haya ni mafanikio kwetu,

Tunawaomba wananchi walitumie dawati la jinsia bila woga na siri zao zitatunzwa kwa kutoa taarifa za kutoroshwa wanafunzi, kuozeshwa na masula ya unyanyasaji endapo yatatokea katika maeneo yao na sisi kama polisi tutawajibika katika eneo letu na kuhakikisha masuala haya yanakwisha kabisa” alisema Chembera.

Aliongeza kuwa kitu kingine kilichosababisha kufanikiwa suala hilo la mimba mashuleni ni kampeni ya “NIACHE NISOME” iliyoanzishwa na mkuu wa wilaya ya Handeni Muhingo Rweyemamu ambayo imekuwa ikiwasisitiza wanafunzi kuzingatia masomo yao na kusoma kwa bidii.

No comments:

Post a Comment