Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Sunday, July 6, 2014

Wananchi wa kata ya Tungi waulalamikio uongozi wa MUROWASA kwa huduma mbovu ya maji safi

WANANCHI wa kata ya tungi manispaa ya morogoro wameulalamikia uongozi wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira MORUWASA kwa kutowapatia huduma nzuri ya upatikanaji wa maji safi katika maeneo yao.

Wakizungumza na kituo hiki wakazi hao wamesema pamoja na na kuwepo na mabomba lakini ni kipindi kirefu sasa wamekuwa wakitumia maji ya vidimbwi yaliyotuama vilivyoachwa na maji ya mvua za masika ambavyo si salama kwa matumizi ya binadamu kutokana na mabomba hayo kutotoa maji.
Voxpops…wananchi

Aidha wamelalamikia pia bei ya Ankara za maji kwani zipo juu tofauti na huduma ya maji wanayoipata nah ii wamesema inatokana na wasoma mita kutoa taarifa za uongo kwa kuandika kiwango kikubwa cha pesa hivyo kuwasababishia baadhi ya watu kuondoa mita majumbani mwao.

Kwa upande wake diwani wa kata ya tungi Deogratius Mzeru amesema kufuati hali hiyo amefika mara nyingi kuonana na uongozi wa muruwasa ili kuzungumzia hatma ya suala la maji katika kata yake ambapo amejibiwa ni jukumu la wananchi kuchangia fedha ili kuunganishiwa bamboo kubwa la maji.
Insert..deogratius Mzeru-diwani kata ya tungi.

Tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama katika manispaa ya morogoro limekuwa kuwa sugu,pamoja na jitihada mbalimbali zinazofanywa na mbunge wa jimbo hilo mheshimiwa abdul azizi abood kulifuatilia kwa ukaribu na hata kulifikisha bungeni.

No comments:

Post a Comment