Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, July 4, 2014

WODC KATA YA LEMBENI YAMPA MTENDAJI WA KIJIJI CHA KISANGARA HADI TAREHE 15 JULAI 2014 MAJI YATOKE LENGURUMO

MWANGA  Kikao cha kujadili maendeleo ya kata ya Lembeni (WODC), wilayani Mwanga mkoani kilimanjaro, kimemwagiza Mtendaji wa kijiji cha kisangara Josephat  Rajabu Kayanda ifikapo tarehe 15 julai 2014 bomba la maji la kitongoji cha Lengurumo liwe limeunganishwa na shimo la choo katika shule ya msingi kisangara liwe limekamilika.

Agizo hilo la kikao cha WODC cha julai 03, mwaka huu limekuja baada ya kubainika kutotekelezwa kwa maazimio ya kikao kilichopita kilichotaka kujua watu waliokata bomba linalopeleka maji kitongoji cha Lengurumo wamepatikana na bomba hilo kuwa limeshafanyiwa matengenezo,ambapo Mtendaji huyo alikiri kutofanikiwa kuwakamata wahusika  na bomba kutofanyiwa matengenezo kutokana na ukosefu wa fedha.

Kayanda amefafanua kwamba imekuwa vigumu kuwakamata waharibifu hao wa miundo mbinu kwa kuwa hufanya uharibifu huo usiku, na kuhusu matengenezo ya bomba amedai hawana pesa ambapo pia hata wilayani alipofuatilia tatizo lilikuwa ni ukosefu wa pesa,naye Bwana maji wa kata ya Lembeni Awadhi Mussa,alipoulizwa alionekana kutoa majibu asiyokuwa na uhakika nayo hali iliyoonyesha kuna uzembe ndani yake.

Wajumbe katika baraza hilo kwa nyakati tofauti,wameonekana kutoridhishwa na majibu ya Bwana maji wa kata aliyeonekana kutokujua hata gharama za matengenezo ya bomba lililovunjika pamoja na sababu za ukosefu wa fedha kwa kile walichohoji kuwa kazi ya bodi ya maji ni nini?ambapo waliwataka siku ya zamu ya maji kuelekea lengurumo ambayo ni kila jumatatu,mabomba yote ya kisangara na mangara yafungwe ili maji yafike.

Aidha kikao hicho cha WODC, kimetaka ratiba ya maji ya kijiji hicho ifuatwe kama inavyostahili na funguo za maji za taasisi ziwekwe ofisi ya kijiiji na kutoa wito katika uongozi wa vijiji vyote vya kata ya lembeni kuwa makini na bodi zao za maji na kuzitaka bodi hizo kuacha ukiritimba katika kuwahudumia wananchi.

Wakazi wa ustawi wa jamii katika kitongoji cha lengurumo hulazimika kutembea umbali wa takribani kilometa saba kufuata maji katika kijiji cha kisangara kwa matumizi ya nyumbani, kwa kutumia usafiri tofauti tofauti ikiwemo punda,bodaboda na magari ;Huku Chuo cha Ustawi wa jamii cha kisangara kikitumia kiasi cha shilingi milioni moja kwa wiki mbili sawa na sh,12milioni kwa miezi sita kununua maji kwa ajili ya matumizi ya chuo hicho.

Mwenyekiti wa kijiji cha kisangara Selemani Said akisoma tarifa ya kijiji katika kikao hicho amesema Waziri wa maji na Mbunge wa wilaya ya mwanga Prof. Jumanne Maghembe aliagiza hadi julai,15 mwaka huu mradi wa visima virefu utakuwa umekamilika na wananchi watapata maji.

No comments:

Post a Comment