Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, August 7, 2014

WANAKIJIJI WAMLALAMIKIA MUWEKEZAJI KWA KUSHINDWA KUTEKELEZA MAKUBALIANO YA MKATABA KWA MIAKA 20



MOSHI wakazi wa kijiji cha Kitandu kata ya Uru kusini wilayani ya Moshi mkoani kilimanjaro wamemtaka mwekezaji wa shamba kubwa la kahawa lenye hekari 555 la kifumbu/kate kutekeleza makubaliano yaliyopo kwenye mkataba wa uwekezaji.

Wananchi hao walitoa agizo hilo katika mkutano  mkuu wa serikali ya kijiji uliofanyika tarehe 5 Augasti 2014 na kuudhuriwa na  wawakilishi wa mwekezaji wa kampuni ya Kilimanjaro  Plantation LTD. (KPL).

Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao Mwenyekiti wa Kijiji hicho Dominick Mushi, alisema kampuni hiyo imeshindwa kutekeleza mkabata huo kwa kushindwa kuwapatia huduma za kijamii wananchi kwa miaka 20.

Mushi alisema baadhi ya huduma hizo ni pamoja na maji, elimu, afya, barabara, ajira kwa wananchi na kudorora kwa ushirikiano kati ya wafanyakazi wa kampuni hiyo na wananchi wa kijiji hicho.

Aidha alisema, kwa muda mrefu serikali ya kijiji ilikuwa inauomba uongozi wa kampuni hiyo kukutana na wananchi kujadili mustakabali wa mkataba huo lakini viongozi wa kampuni wamekuwa hawatoi ushirikiano.

Alisema kwa zaidi ya miaka 20 ni mara ya kwanza kwa viongozi wa kamapuni hiyo kukaa na wananchi na kusikiliza kero zao zinazo wakabili likiwemo suala zima la maendeleo.

Kwa upande wake mwakilishi wa kampuni hiyo Jacob De Haan aliahidi  kuwasilisha hoja za wananchi hao kwa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo Volker Schuckert ambaye kwa sasa yuko nchini Ujerumani kwa mapumziko na kwamba  matumaini yake kuwa zitafanyiwa kazi kwa mujibu wa mkataba.

Mkuu wa kitengo cha ulinzi na usalama wa kampuni hiyo Shaaban Deogratius alikiri uhusiano mbaya uliopo kati ya pande hizo na kuaahidi kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano na kuondoa tofauti zilizojitokeza.

Shaaban alisema, katika hatua za awali aliahidi ajira 25 za ulinzi kwa vijana watakaomaliza mafunzo ya mgambo katika kijiji hicho ili kuziba pengo la walinzi waliopo ambao baadhi yao ni wazee na wengine hawana sifa.

Nao baadhi ya wananchi hao walikiomba chama cha msingi cha ushirika mkoani  Kilimanjaro kurejea katika mkataba huo upya kutokana na kwamba awali walitiliana saini na kampuni ijulikanayo kwa jina la T-CHIBO, lakini sasa kampuni iliyopo ni kilimanjaro Planters ltd.

No comments:

Post a Comment