Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, September 8, 2014

ALIYEKUWA MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WAZAZI MKOANI KILIMANJARO ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE 2015


MOSHI aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi, (CCM), mkoani Kilimanjaro, Thomas Ngawaiya, ametangaza nia yake ya kugombea kiti cha ubunge cha Moshi Vijijini, mkoani Kilimanjaro, katika uchaguzi mkuu wa 2015.

Ngawaiya ambae aliwahi kuwa mbunge wa jimbo hilo kati ya mwaka 2000 na 2005, ametangaza nia yake hiyo, akiwa nyumbani kwake Kibosho, ambapo amesema lengo kuu la nia yake hiyo ni kuharakisha maendeleo katika jimbo hilo.

Amesema mwaka 2005 hakufanya hivyo kwa vile wakati akipewa ushauri huo tayari alishaamua kugombea ubunge wa jimbo la Moshi Mjini na kushika nafasi ya tatu katika kura za maoni ndani ya CCM.

Ngawaiya amesema kuwa kingine kilichompa msukumo wa kufanya hivyo ni kuwa jimbo la Moshi Vijijini limekosa mtetezi wa ngazi hiyo haswa katika sekta ya kilimo cha kahawa na kwamba ameazimia kuhakikisha zao hilo linarudia hadhi yake ya awali kwa manufaa ya wakulima wake.

Aidha amesema aliasisi mradi wa ujenzi wa barabara za maeneo ya jimbo hilo kwa kiwango cha lami na kwamba wananchi wa eneo hilo ambao ni wapiga kura ndiyo mashahidi wake.

Jimbo hilo kwa sasa linashikiliwa na Dk. Cyril Chami, wa CCM; mbali na Ngawaiya, wengine ambao wameshaonyesha nia ya kuwania kiti hicho ni pamoja na aliekuwa mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Benno Malisa, ambapo taarifa zingine zisizo rasmi zinaonyesha ya kuwa mbunge wa viti maalum
kupitia Chadema,Lucy Owenya, pia anatarjia kuwania kiti hicho.

No comments:

Post a Comment