Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Tuesday, September 9, 2014

MTU MMOJA ANAYESADIKIKA NI JAMBAZI AMEUWAWA KWA RISASI KATIKA ENEO LA NJIAPANDA YA HIMO

MOSHI mtu mmoja kati ya watatu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi amemiminiwa risasi kadhaa mwilini na kufariki dunia papo hapo, kwa kile kilichodaiwa kuwa alijibizana kwa kurushiana risasi za moto na askari wa jeshi la polisi wa kituo cha polisi Himo, katika eneo la njia panda Himo, mkoani Kilimanjaro. Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Robert Boas, alisema aliyeuawa hajatambulika kwa jina lakini inasadikiwa kuwa ni raia wa nchi jirani, ambapo kamanda huyo hakuwa tayari kuitaja nchi hiyo kwa sababu za kiupelelezi. Amewataja wanaoshikiliwa na jeshi hilo kuwa ni, Edimund Ludoviki (36), mkazi wa Rombo, ambaye amekuwa akihusishwa na matukio mbalimbali ya unyang’anyi kwa kutumia silaha za moto, katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro na Endrick Ngomuo (30), ambaye ni mkazi wa makuyuni himo. Marehemu huyo baada ya kuuawa alipekuliwa na kukutwa na bastora aina ya Cheinis ikiwa na risasi 12, pamoja na kofia za kuziba uso (mask). Akizungumzia mazingira ya tukio hilo, kamanda Boas amesema watu hao walikutwa wakiwa bar inayoitwa Gozar inayomilikiwa na Mery Mauki, baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema za kuwepo kwa majambazi hao ambayo walikuwa wakijiandaa kupora.

No comments:

Post a Comment