Banner

FOLLOW US FACEBOOK
propertyfinder.co.tz
Wednesday, August 27, 2014
ZAIDI YA MILIONI 120 ZINAHITAJIKA ILI KUFANIKISHA “Mount Kilimanjaro Festival”
KILIMANJARO zaidi ya Shilingi Milioni 120 zinahitajika ili kukamilisha Tamasha la Biashara, Utamaduni na Michezo (Mount Kilimanjaro Festival) linalotarajiwa kufanyika Desemba 17-23 mwaka huu mkoani Kilimanjaro.
Pia Mkuu huyo wa Mkoa aliongeza kusema katika ufunguzi wake mwaka huu watakuwa na msanii maarufu wa nyimbo ambaye hakutaka jina lake litajwe na timu ya daraja la kwanza au Ligi kuu itayoweza kutoa burudani kwa ajili ya kuhamasisha wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandilizi ya Tamasha hilo Patrick Boisafi alisema Desemba 17-23 ni kilele cha shughuli nzima itakayoanza kufanyika katika wilaya nane za mkoa wa Kilimanjaro ili kutafuta vikundi na timu mbalimbali.
“Kibiashara tamasha hili litasaidia kukuza uchumi, utamaduni na michezo, pia vitatoa hamasa kwa vijana chipukizi lakini litahusisha vikundi na timu za serikali za mitaa, ili kunogesha zaidi, hivyo maandalizi yanatakiwa kuanzia wilayani hadi siku ya kilele”.
Aidha alisema vikundi na timu hizo zinatakiwa kuandaliwa ipasavyo ikiwemo michezo ya bao, ngoma, kukimbia kwa magunia, kuvuta kamba, mpira wa pete, mpira wa miguu na mpira wa wavu.
Kauli mbiu ya Mt. Kilimanjaro Festival ni “ Biashara, Utamaduni na Michezo, kujenga uchumi wa Kilimanjaro”.
Na Jabir Johnson
Monday, August 25, 2014
Mkurugenzi mtendaji wa Panone "Patrick Ngiloi Ulomi" akiipokea timu ya Real Madrid
Mkurugenzi mtendaji wa Panone Patrick Ngiloi Ulomi akimkabidhi zawadi Waziri
wa habari, vijana, utamaduni na michezo Dkt. Fenella Mukangara ili aweze kuikabidhi timu ya Real Madrid
Mkurugenzi mtendaji wa Panone Patrick Ngiloi Ulomi wakiwa katika hifadhi ya Mlima Kilimanjaro ( KINAPA)
Friday, August 22, 2014
ZIARA YA MAGWIJI WA MPIRA ULIMWENGUNI REAL MADRID MKOANI KILIMANJARO

Kuanzia
kushoto, Luis Figo, Zinedine Zidane na Ronaldo de Lima enzi hizo
wakicheza Real Madrid - See more at:
http://shaffihdauda.com/?p=3927#sthash.mdYMdq4X.dpuf
Kuanzia
kushoto, Luis Figo, Zinedine Zidane na Ronaldo de Lima enzi hizo
wakicheza Real Madrid - See more at:
http://shaffihdauda.com/?p=3927#sthash.mdYMdq4X.dpuf
Kutoka kulia ni Ronaldo De Lima, Zinedine Zidane na Luis Figo, enzi wakichezea Real MAdrid
Kuanzia
kushoto, Luis Figo, Zinedine Zidane na Ronaldo de Lima enzi hizo
wakicheza Real Madrid - See more at:
http://shaffihdauda.com/?p=3927#sthash.mdYMdq4X.dpuf
Kuanzia
kushoto, Luis Figo, Zinedine Zidane na Ronaldo de Lima enzi hizo
wakicheza Real Madrid - See more at:
http://shaffihdauda.com/?p=3927#sthash.mdYMdq4X.dpuf
MOSHI
timu ya Real Madrid ya nchini Hispania, inatarajia kuwasili mkoani
Kilimanjaro, Agosti 24, mwaka 2014 lengo likiwa ni kutangaza fursa za
utalii zilizopo mkoani Kilimanjaro hususani katika mlima Kilimanjaro.
Akitoa taarifa kwa wanahabari mkoani Kilimanjaro, mkuu wa mkoa wa
Kilimanjaro, Leonidas Gama, alisema ziara ya wachezaji hao itatoa mwanya
kwa wachezaji wengine kuja hapa nchini Tanzania na kuweza kuzitembelea
hifadhi zilizopo hapa nchini.
Alisema uongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kwa kushirikiana na wadau wa michezo wamejiandaa vyema katika kuwapokea wachezaji hao, na kuongeza kuwa mkoa umejiandaa vyema katika kuwakarimu wachezaji hao wa Real Madrid.
Gama alisema kuwa licha ya wachezaji hao kuja na kutembelea hifadhi ya mlima Kilimanjaro pia itatoa fursa ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo mkoani Kilimanjaro, na kwamba mkoa umeandaa ratiba ambayo itawafikisha hadi kwenye mlima Kilimanjaro na kupata maelezo kuhusu mlima mrefu kuliko yote barani Afrika.
Pia mkuu wa mkoa alisema baada ya kufika eneo la mlima Kilimanjaro, watapata fursa ya kupanda kwa umbali kidogo ili kujionea mandhari ya mlima huo jinsi ulivyo kisha kupata maelezo ya jinsi safari ya kuanza kuupanda mlima huo inavyofanyika.
Aidha alifafanua kuwa uongozi wa mkoa umeuagiza uongozi wa hifadhi ya mlima Kilimanjaro (KINAPA), kuandaa maelezo yatakayowawezesha wachezaji hao kushawishika kurudi tena kama watalii. Kwa mujibu wa ratiba ya ziara ya wachezaji hao baada ya kupanda mlima Kilimanjaro, watapata chakula cha mchana kabla ya kurudi mjini Moshi ambapo wanatarajia kuwa wageni rasmi katika mechi ya kirafiki kati ya mabingwa wa mkoa wa Kilimanjaro Panone FC na timu ya soka ya Machava ya mjini Kilimanjaro.
Alisema uongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kwa kushirikiana na wadau wa michezo wamejiandaa vyema katika kuwapokea wachezaji hao, na kuongeza kuwa mkoa umejiandaa vyema katika kuwakarimu wachezaji hao wa Real Madrid.
Gama alisema kuwa licha ya wachezaji hao kuja na kutembelea hifadhi ya mlima Kilimanjaro pia itatoa fursa ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo mkoani Kilimanjaro, na kwamba mkoa umeandaa ratiba ambayo itawafikisha hadi kwenye mlima Kilimanjaro na kupata maelezo kuhusu mlima mrefu kuliko yote barani Afrika.
Pia mkuu wa mkoa alisema baada ya kufika eneo la mlima Kilimanjaro, watapata fursa ya kupanda kwa umbali kidogo ili kujionea mandhari ya mlima huo jinsi ulivyo kisha kupata maelezo ya jinsi safari ya kuanza kuupanda mlima huo inavyofanyika.
Aidha alifafanua kuwa uongozi wa mkoa umeuagiza uongozi wa hifadhi ya mlima Kilimanjaro (KINAPA), kuandaa maelezo yatakayowawezesha wachezaji hao kushawishika kurudi tena kama watalii. Kwa mujibu wa ratiba ya ziara ya wachezaji hao baada ya kupanda mlima Kilimanjaro, watapata chakula cha mchana kabla ya kurudi mjini Moshi ambapo wanatarajia kuwa wageni rasmi katika mechi ya kirafiki kati ya mabingwa wa mkoa wa Kilimanjaro Panone FC na timu ya soka ya Machava ya mjini Kilimanjaro.
DIWANI WA KATA YA MASAMA ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA HAI.
HAI
baraza la Madiwani la halmashauri ya Wilaya ya Hai, Mkoani
Kilimanjaro limemchagua Ally Mwanga ambae ni Diwani wa kata ya
Masama Mashariki (CCM) kuwa makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo
kwa kipindi cha kuanzia Julai 2014 hadi June 2015.
Mwanga alichaguliwa kwa kupigiwa kura za siri za ndio au hapana baada
ya mgombea wa Chama cha Demokransia na Maendeleo (CHADEMA) kujitoa
kutokana na maridhiano walikubaliana wajumbe wa baraza hilo linaloundwa
na vyama viwili vya Siasa vya CCM na CHADEMA.
Uchaguzi huo wa kumchagua makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo
ulifanyika katika ukumbi wa Halamashauri ambapo vyama hivyo viwili
vilikubaliana nafasi ya makamu mwenyekiti iendelee kushikiliwa na diwani
wa CCM kutokana na kuongozwa na Mwenyekiti anayetoka CHADEMA.
Awali akitangaza matokeo hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo
Melekzedeck Humbe alisema Mwanga alipata kura 18 kati ya 19 zilizopigwa
huku moja ikiharibika.
Baraza hilo la madiwani pia liliwachagua wajumbe na wenyeviti
mbalimbali wa kamati watakao ongoza kwa pindi cha mwaka mmoja
cha kuanzia Agosti 2014 hadi June 2015.
Thursday, August 21, 2014
Downloa na Kusikiliza Wimbo wa ODEO ft. RUFF G - Wanibembeleza, (NOIZ)
Muite ODEO, Msanii chipukizi katika Game la muziki anakuja na wimbo "WANIBEMBELEZA" akiwa na Ruff G toka Nyutro Fellaz kwenye Chorus, bofya HAPA kupata WIMBO na kwa mahojiano/mawasiliano zaidi check na ODEO kwa nambari +255 757 041 671.
WATANZANIA WASHAURIWA KUJIENDELEZA KIELIMU KWA KUPITIA VYUO VIKUU HURIA
Wananchi, watumishi wa umma na mashirika binafsi hapa nchini Tanzania wameshauriwa kujiunga katika vyuo
vikuu huria vilivyopo hapa nchini ili waweze kujiongezea elimu itakayo wawezesha
kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi sambamba na kumudu ushindani wa soko la ajira.
Rai hiyo imetolewa na rais wa wanafunzi wa chuo kikuu huria cha mjini Moshi Bw. Adinani Kingazi ,walipotembelewa chuoni hapo na makamu
mkuu wa chuo kikuu huria cha Tanzania Bw. Tolly Mbwette, ambapo amesema jamii
inatakiwa kutambua kuwa ,kuna umuhimu wakujiendeleza kielimu.
Bw. Kingazi alisema njia pekee ambayo itakayoweza kumkomboa
mtumishi wa umma ama sekta binafsi kukabiliana ipasavyo katika soko la ajira
ni kusoma katika chuo kikuu huria, ambapo kinampa fursa ya kusoma bila kuathiri
shughuli zake za kiutendaji.
Makamu mkuu
wa chuo kikuu huria nchini Bw. Tolly Mbwette alisema serikali imeanza kuboresha
baadhi miundombinu ikiwemo majengo katika vyuo vikuu huria hapa nchini pia katika kutekeleza
mpango wa matokeo makubwa sasa ina mpango maalumu wa kuhakikisha kuwa inajenga vyuo vikuu huria nchi nzima.
Tuesday, August 19, 2014
MAJAMBAZI WAMUUA MLINZI KIKATILI NA KUPORA MALI
MOSHI watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wamempiga mlinzi wa jengo la Lyamuya Constraction, Musa Muhamed (52) mkazi wa Mabogini, na kitu kibutu kichwani na kusababishia kufariki dunia, pamoja na kuvunja maduka mawili yaliyopo katika jengo hilo la Lyamuya Constraction.
Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro Robert Boaz, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba lilitokea usiku wa kuamkia agusti 18 mwaka 2014 , katika mtaa wa kaunda, manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, ambapo watu hao waliingia katika jengo hilo na kumpiga mlizi huyo na kitu kizito kichwani.
Boaz alisema baada ya kumpiga mlizi huyo watu hao walim'buruta hadi sehemu ambapo magari ya jengo hilo huegeshwa na kuutelekeza mwili wa marehemu.
Alisema watu hao baada ya kufanya unyama huo walivunja maduka mawili ambapo waliiba tarakilishi “Computer” mbili na vitu mbalimbali ambavyo thamani yake hajaweza kufahamika kwa haraka.
Kamanda Boaz, alisema walivunja duka la mimea na mifugo na kuiba tarakilishi “Computer” na vitu vingine ambavyo havija tambuliwa na wahusika ambapo alisema pia walivunja duka la vifaa vya umeme ambapo pia waliiba tarakilishi “Computer” na vifaa mbalimbali vya umeme.
Boaz alisema hakuna anaeshikiliwa hadi sasa na kwamba uchunguzi unaendelea ili kuweza kuwatia nguvuni waliofanya tukio hilo, na kwamba mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya mkoa ya Mawenzi.
Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro Robert Boaz, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba lilitokea usiku wa kuamkia agusti 18 mwaka 2014 , katika mtaa wa kaunda, manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, ambapo watu hao waliingia katika jengo hilo na kumpiga mlizi huyo na kitu kizito kichwani.
Boaz alisema baada ya kumpiga mlizi huyo watu hao walim'buruta hadi sehemu ambapo magari ya jengo hilo huegeshwa na kuutelekeza mwili wa marehemu.
Alisema watu hao baada ya kufanya unyama huo walivunja maduka mawili ambapo waliiba tarakilishi “Computer” mbili na vitu mbalimbali ambavyo thamani yake hajaweza kufahamika kwa haraka.
Kamanda Boaz, alisema walivunja duka la mimea na mifugo na kuiba tarakilishi “Computer” na vitu vingine ambavyo havija tambuliwa na wahusika ambapo alisema pia walivunja duka la vifaa vya umeme ambapo pia waliiba tarakilishi “Computer” na vifaa mbalimbali vya umeme.
Boaz alisema hakuna anaeshikiliwa hadi sasa na kwamba uchunguzi unaendelea ili kuweza kuwatia nguvuni waliofanya tukio hilo, na kwamba mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya mkoa ya Mawenzi.
Friday, August 15, 2014
WAZAZI WATAKIWA KUWA WAZALENDO KATIKA KULIPA ADA KWA AJILI YA WATOTO WAO
HAI wananchi wa wilaya ya Hai mkoani
Kilimanjaro wametakiwa kuwa wazalendo wa katika kulipa ada ya shule kwa watoto
wao ili kuwapa watoto fursa ya kupata elimu kama ilivyo kusudiwa.
Swala hilo muhimu liliongelewa na Afisa Elimu sekondari wa wilaya ya Hai, Bw. Julius Kakyama, alipokuwa akizungumza na wananchi wa kata ya kibaoni kwenye kikao kilicho fanyika hivi karibuni katika ofisi ya mtaa wa kibaoni kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi.
Kakyama alisema kuwa wananchi wengi wamekuwa wakiwapeleka watoto wao shuleni kwa lengo na kusoma lakini likija suala la kuchangia chakula mashuleni wamekuwa wakaidi sana, jambo hilo la kutokutaka kutoa michango ya shule linarudisha elimu nyuma, hivyo amewaomba wazazi wilayani humo kuchangia chakula kwa wingi mashuleni ili wanafunzi waweze kufaulu, kwani wanafunzi kukosa chakula kunawafanya kushindwa kufanya vizuri katika masomo yao.
Alisema kuwa anatambua mchango mkubwa toka serikalini wa ujenzi wa shule na mabweni kwa shule ya sekondari Hai Day unaoendelea kufanyika pamoja na juhudi za wananchi katika kutoa michango yao kufanikisha ujenzi huo.
Akizungumzia suala la maabara katika shule ya sekondari Boma alisema kuwa wametoa ushirikiano katika ujenzi kwa fedha za TASAF mwaka 2007 na kukamilisha madarasa.
Ameongeza pia mwaka 2011 walitumia fedha zilizo tolewa na TASAF na kujenga vyoo vya shule ambapo pia vilikamilika na kusema kuwa katika suala la ujenzi wa maabara kuna mpango unaoandaliwa na halmashauri ya kuandika barua kwa watendaji kata ili waweze kufanyia mchakato suala hilo la ujenzi wa maabara.
WANANCHI WALALAMIKIA HUDUMA MBOVU ZA AFYA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA
HAI wananchi wa mtaa wa kibaoni, kata ya Hai mjini, wilayani Hai mkoani Kilimanjaro
wamelalamikia utaratibu na huduma zinazotolewa na hosipitali ya wilaya
ya Hai kuwa haziridhishi na wananchi hao kulalamikia kudorora kwa huduma muhimu kama ya afya.
Wananchi hao wametoa malalamiko hayo hivi karibuni wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika ofisi ya Mtaa wa Kibaoni na kuhudhuriwa na mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga, pamoja na wakuu wa idara wa wilaya ya Hai, katika kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Baadhi ya kero ambazo wananchi hao walizitoa mbele ya mkuu wa wilaya ni pamoja na lugha chafu kwa baadhi ya wauguzi, muda mrefu wa kusubiri huduma mapokezi pamoja na ukosefu wa dawa tatizo linalo leta kero kwa wagonjwa.
Awali akisoma risala kwa mkuu wa wilaya mwenyekiti wa mtaa wa kibaoni ambaye ni diwani wa viti maalumu Amina Swai, alisema kuwa wagonjwa wamekuwa wakikosa dawa hospitalini hapo na kuelekezwa kununua dawa hizo katika maduka ya dawa yanayomilikiwa na watu binafsi.
Mwakilishi wa mganga mkuu wa hospitali ya wilaya Felista Ritte, alikiri kuwepo kwa kero hizo hospitalini hapo na kusema kuwa tayari kuna watu na kitengo maalumu cha kusikiliza kero na kuzitatua ikiwa ni pamoja na kuwachukulia sheria kali kwa wauguzi na madaktari watakao kiuka wajibu wao kwa wagonjwa.
Wananchi hao wametoa malalamiko hayo hivi karibuni wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika ofisi ya Mtaa wa Kibaoni na kuhudhuriwa na mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga, pamoja na wakuu wa idara wa wilaya ya Hai, katika kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Baadhi ya kero ambazo wananchi hao walizitoa mbele ya mkuu wa wilaya ni pamoja na lugha chafu kwa baadhi ya wauguzi, muda mrefu wa kusubiri huduma mapokezi pamoja na ukosefu wa dawa tatizo linalo leta kero kwa wagonjwa.
Awali akisoma risala kwa mkuu wa wilaya mwenyekiti wa mtaa wa kibaoni ambaye ni diwani wa viti maalumu Amina Swai, alisema kuwa wagonjwa wamekuwa wakikosa dawa hospitalini hapo na kuelekezwa kununua dawa hizo katika maduka ya dawa yanayomilikiwa na watu binafsi.
Mwakilishi wa mganga mkuu wa hospitali ya wilaya Felista Ritte, alikiri kuwepo kwa kero hizo hospitalini hapo na kusema kuwa tayari kuna watu na kitengo maalumu cha kusikiliza kero na kuzitatua ikiwa ni pamoja na kuwachukulia sheria kali kwa wauguzi na madaktari watakao kiuka wajibu wao kwa wagonjwa.
Ameongeza kwa kuwataka wananchi hao kuwa wazalendo wa kuepuka gharama kubwa za kulipia matibabu kwa kuwataka kukata bima ya afya ili kuwarahisishia kupata matibabu.
Friday, August 8, 2014
KESI YA MAREHEMU MTOTO "NASRA RASHID MVUNGI" YAPIGWA TENA TAREHE
Watuhumiwa Bw. Rashid Mvungi pamoja na
waliokuwa walezi wake, Bi. Mariam Said na mumewe Mtonga Omary, wakiwa mahakamani.
Umati wa watu waliokuja kusikiliza kesi ya marehemu mtoto Nasra, wakiwa nje ya mahakama.
MOROGORO washtakiwa watatu wanaokabiliwa na mashtaka ya mauaji dhidi ya mtoto Nasra Rashid Mvungi, wamelazimika kubadilishiwa hakimu baada ya hakimu ambaye kesi yao imekuwa ikifikishwa mbele yake kwaajili ya kutajwa, kupata dharura na kutokuwepo mahakamani hapo.
MOROGORO washtakiwa watatu wanaokabiliwa na mashtaka ya mauaji dhidi ya mtoto Nasra Rashid Mvungi, wamelazimika kubadilishiwa hakimu baada ya hakimu ambaye kesi yao imekuwa ikifikishwa mbele yake kwaajili ya kutajwa, kupata dharura na kutokuwepo mahakamani hapo.
Washtakiwa hao ambao kesi yao
imekuwa ikifikishwa na kutajwa, mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya
hakimu mkazi mkoa wa Morogoro, Mary Moyo, wamelazimika kupandishwa
kizimbani mbele ya Hakimu Agripina Kimanze na kusomewa mashtaka yao, baada ya
hakimu Moyo kutokuwepo mahakamani hapo.
Kufuatia hali hiyo, washtakiwa hao
walichelewa kupanda kizimbani tofauti na nyakati nyingine, hali iliyoonekana
huenda ilisababishwa na mabadiliko hayo ya kukosekana kwa hakimu husika.
Mwendesha Mashtaka wa Polisi
Aminatha Mazengo, aliiambia mahakama kuwa upelelezi wa shauri hilo bado
haujakamilika na kwamba jalada bado lipo kwa Mwanasheria mkuu wa Serikali,
hivyo kuiomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo.
Mahakama imeridhia ombi hilo, na
kupanga Agosti 20 mwaka 2014, kufikishwa tena kwa kesi hiyo kwaajili ya kutajwa,
kutokana na mahakama hiyo kukosa uwezo kisheria kusikiliza shtaka la mauaji huku washtakiwa wakirudishwa rumande kutokana
na kesi hiyo kutokuwa na dhamana.
Kesi hiyo ya mauaji inawakabili
washtakiwa watatu akiwemo baba mzazi wa mtoto Nasra, Bw. Rashid Mvungi pamoja na
waliokuwa walezi wake, Bi. Mariam Said Na mumewe Mtonga Omary, ambao awali
walikuwa wakikabiliwa na shtaka la kula njama na kufanya vitendo vya ukatili
dhidi ya Mtoto Nasra Mvungi kabla ya baadaye mashtaka yao kubadilishwa na kuwa
ya mauaji baada ya mtoto huyo kufariki dunia katika hospitali ya Taifa ya
Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa matibabu.
AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA MAKOSA YA UKATILI KWA MFANYAKAZI WAKE WA NDANI
KILIMANJARO mkazi mmoja wa Singida mjini aliyefahamika kwa jina la Jackline Kweka (30) jana alipandishwa Mahakama ya wilaya ya Hai akikabiliwa na tuhuma za kumfanyia ukatili mfanyakazi wake
wa ndani mwenye umri wa miaka 15.
Inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa akimpiga mfanyakazi wake huyo sehemu mbalimbali za mwili ikiwamo kumvuta nyama za siri kwa kutumia plaizi.
Baada ya tuhuma hizo kuibuliwa na raia wema mtuhumiwa huyo alitoroka kutoka mkoani Singida na kukimbilia katika kijiji cha Narumu wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro alikokamatiwa baada ya taarifa kuvuja.
Mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani mbele ya hakimu mkazi, mfawidhi wa wilaya, Denis Mpelembwa na kukanusha mashitaka dhidi yake. Hati ya mashitaka hayo ni ya awali ili kuruhusu polisi kutoka Singida kwenda kumchukua mtuhumiwa huyo.
Akisoma mashitaka Mwendesha Mashitaka wa polisi, inspekta Marwa Mwita alidai mtuhumiwa huyo alitenda makosa hayo Julai mwaka 2014, kwa siku tofauti tofauti.
Mtuhumiwa huyo alikanusha mashitaka hayo na amerudishwa rumande hadi Agosti 21 mwaka 2014, wakati ukisubiriwa utaratibu wa kumsafirisha kwenda mkoani Singida.
Msichana anayedaiwa kufanyiwa ukatili huo alilazwa katika hospitali ya wilaya ya Hai kwa Matibabu na taarifa zinadai amepoteza uwezo wa kusikia na hapati tene siku zake za hedhi.
Inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa akimpiga mfanyakazi wake huyo sehemu mbalimbali za mwili ikiwamo kumvuta nyama za siri kwa kutumia plaizi.
Baada ya tuhuma hizo kuibuliwa na raia wema mtuhumiwa huyo alitoroka kutoka mkoani Singida na kukimbilia katika kijiji cha Narumu wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro alikokamatiwa baada ya taarifa kuvuja.
Mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani mbele ya hakimu mkazi, mfawidhi wa wilaya, Denis Mpelembwa na kukanusha mashitaka dhidi yake. Hati ya mashitaka hayo ni ya awali ili kuruhusu polisi kutoka Singida kwenda kumchukua mtuhumiwa huyo.
Akisoma mashitaka Mwendesha Mashitaka wa polisi, inspekta Marwa Mwita alidai mtuhumiwa huyo alitenda makosa hayo Julai mwaka 2014, kwa siku tofauti tofauti.
Mtuhumiwa huyo alikanusha mashitaka hayo na amerudishwa rumande hadi Agosti 21 mwaka 2014, wakati ukisubiriwa utaratibu wa kumsafirisha kwenda mkoani Singida.
Msichana anayedaiwa kufanyiwa ukatili huo alilazwa katika hospitali ya wilaya ya Hai kwa Matibabu na taarifa zinadai amepoteza uwezo wa kusikia na hapati tene siku zake za hedhi.
MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AWASHAURI WANANCHI KUJIWEKEA AKIBA YA CHAKULA
KILIMANJARO serikali mkoani Kilimanjaro imewataka wananchi kujiwekea
akiba ya chakula katika kipindi hichi cha mavuno na kuacha kutumia nafaka kwa
kutengenezea pombe za kienyeji, lengo likiwa ni kukabiliana na kipindi cha njaa.
Mkuu wa mkoa wa kilimnjaro Leonidas Gama, aliyasema hayo
wakati akizungumza na mmoja muandishi wa mtandao huu jana
Mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro ambapo alisema hali ya kilimo na upatikanaji wa
chakula ni ya kuridhasha.
Alisema mkoa wa Kilimanjaro baadhi ya wilaya zake zimekuwa zikikabiliwa na
njaa kutokana na wananchi kutokuwa na
desturi ya kujiwekea akiba ya chakula katika kipindi cha mavuno na kutumia
nafaka katika utengenzaji wa pombe za kienyeji.
Alisema mkoa
ulijiwekea malengo ya kuvuna na kukusanya zaidi ya tani Milioni 1.9 katika
kipindi cha mwaka 2013/2014 na kwamba
hali ya upatikaji wa chakula ni ya kuridhisha ambapo katika
kipindi cha mwaka 2014 wanatarajia kuvuna kuvuka lengo hilo.
Aidha aliziagiza halmashauri za wilaya kupitia wataalamu wa kilimo mkoani Kilimanjaro
kuwaelimisha wananchi juu ya njia bora za kuhifadhi mazao ili kusaidia vyakula hivyo kuto haribika
kwa haraka.
Thursday, August 7, 2014
MKOA WA KILIMANJARO UMEFANIKIWA KUJENGA MAABARA ZAIDI YA 130
KILIMANJARO maabara zaidi ya 130 zimejengwa katika mkoa wa Kilimanjaro kwenye shule mbalimbali za sekondari, kwa lengo la kuboresha masomo ya sayansi katika shule hizo na mkoa huo kwa ujumla.
Hayo yalielezwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama, wakati akizungumza na wanahabari kuhusiana na agizo la Rais wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, lililowataka viongozi wa mikoa yote Tanzania kuhakikisha kila shule ya sekondari inakuwa na maabara.
Mkuu huyo wa mkoa wa Kilimanjaro alisema katika kutekeleza mpango huo kumekuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ile ya wananchi kuwa na ugumu wa kutokuwa na ushirikiano katika ujenzi wa maabara hizo ili kufanikisha zoezi hilo.
Aidha Gama aliwataka wananchi kuona umuhimu wa kuchangia miradi ya maendeleo katika maeneo yao ikiwemo sekta ya elimu na kwamba mbali na juhudi za serikali michango inayotolewa na wananchi ni muhimu kwa ajili ya maendeleo.
Alisisitiza na kutoa wito kwa wanafunzi kuhakikisha wanajituma katika elimu ili kuenzi juhudi zinazofanywa na serikali pamoja na wananchi katika kuchangia miradi ya elimu.
Hayo yalielezwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama, wakati akizungumza na wanahabari kuhusiana na agizo la Rais wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, lililowataka viongozi wa mikoa yote Tanzania kuhakikisha kila shule ya sekondari inakuwa na maabara.
Mkuu huyo wa mkoa wa Kilimanjaro alisema katika kutekeleza mpango huo kumekuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ile ya wananchi kuwa na ugumu wa kutokuwa na ushirikiano katika ujenzi wa maabara hizo ili kufanikisha zoezi hilo.
Aidha Gama aliwataka wananchi kuona umuhimu wa kuchangia miradi ya maendeleo katika maeneo yao ikiwemo sekta ya elimu na kwamba mbali na juhudi za serikali michango inayotolewa na wananchi ni muhimu kwa ajili ya maendeleo.
Alisisitiza na kutoa wito kwa wanafunzi kuhakikisha wanajituma katika elimu ili kuenzi juhudi zinazofanywa na serikali pamoja na wananchi katika kuchangia miradi ya elimu.
WANAKIJIJI WAMLALAMIKIA MUWEKEZAJI KWA KUSHINDWA KUTEKELEZA MAKUBALIANO YA MKATABA KWA MIAKA 20
MOSHI wakazi wa
kijiji cha Kitandu kata ya Uru kusini wilayani ya Moshi mkoani kilimanjaro
wamemtaka mwekezaji wa shamba kubwa la kahawa lenye hekari 555 la kifumbu/kate
kutekeleza makubaliano yaliyopo kwenye mkataba wa uwekezaji.
Wananchi hao walitoa agizo hilo katika
mkutano mkuu wa serikali ya kijiji uliofanyika tarehe 5 Augasti 2014 na
kuudhuriwa na wawakilishi
wa mwekezaji wa kampuni ya Kilimanjaro Plantation LTD. (KPL).
Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao
Mwenyekiti wa Kijiji hicho Dominick Mushi, alisema kampuni hiyo imeshindwa
kutekeleza mkabata huo kwa kushindwa kuwapatia huduma za kijamii wananchi kwa
miaka 20.
Mushi alisema baadhi ya huduma hizo ni
pamoja na maji, elimu, afya, barabara, ajira kwa wananchi na kudorora kwa
ushirikiano kati ya wafanyakazi wa kampuni hiyo na wananchi wa kijiji hicho.
Aidha alisema, kwa muda mrefu serikali
ya kijiji ilikuwa inauomba uongozi wa kampuni hiyo kukutana na wananchi
kujadili mustakabali wa mkataba huo lakini viongozi wa kampuni wamekuwa hawatoi
ushirikiano.
Alisema kwa zaidi ya miaka 20 ni mara ya
kwanza kwa viongozi wa kamapuni hiyo kukaa na wananchi na kusikiliza kero zao
zinazo wakabili likiwemo suala zima la maendeleo.
Kwa upande wake mwakilishi wa kampuni
hiyo Jacob De Haan aliahidi kuwasilisha hoja za wananchi hao kwa
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo Volker Schuckert ambaye kwa sasa yuko nchini
Ujerumani kwa mapumziko na kwamba matumaini yake kuwa zitafanyiwa kazi
kwa mujibu wa mkataba.
Mkuu wa kitengo cha ulinzi na usalama wa
kampuni hiyo Shaaban Deogratius alikiri uhusiano mbaya uliopo kati ya pande
hizo na kuaahidi kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano na kuondoa tofauti
zilizojitokeza.
Shaaban alisema, katika hatua za awali
aliahidi ajira 25 za ulinzi kwa vijana watakaomaliza mafunzo ya mgambo katika
kijiji hicho ili kuziba pengo la walinzi waliopo ambao baadhi yao ni wazee na
wengine hawana sifa.
“KIRUA VUNJO NORTH AMCOS” Yatarajia Kukusanya Shilingi Milioni 4.8 Kwa Mwaka 2014/2015
“Ziada hii itatokana na
mapato ya jumla ya zaidi ya shilingi milioni 15 tunayotarajia kuyapata katika
kipindi hiki”, alisema na kuongeza kuwa wanachama wa chama hicho tayari
wameridhia kujiunga na mfumo mpya wa kukusanya kahawa kwa kujitegemea.
Subscribe to:
Posts (Atom)